Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko (kulia) akizungumza na wafanyakazi wa Ofisi ya Madini Dodoma, alipowatembelea akiwa katika ziara ya kazi, Machi 22 mwaka huu.

Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko, akisalimiana na wafanyakazi wa Ofisi ya Madini Dodoma, alipowasili katika Ofisi hiyo akiwa katika ziara ya kazi, Machi 22 mwaka huu.

 Shughuli za uchimbaji madini ya nakshi zikiendelea katika Mgodi uliopo Ntyuka Dodoma, wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko (hayupo pichani) mgodini hapo Machi 22 mwaka huu.

Sehemu ya shehena ya mawe ya nakshi aina ya Graphite. Taswira hii ilichukuliwa Machi 22 mwaka huu wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko (hayupo pichani) katika Mgodi uliopo Itiso wilayani Chamwino.


Ø Yachangia bilioni 7.1 mrabaha 2016/17
Ø Asema usimamizi mzuri unaweza kukuza mchango huo kufikia bilioni 15 kwa mwaka.

Na Veronica Simba – Dodoma
Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko, amesema kuwa madini ya ujenzi na viwanda yanaipatia Serikali fedha nyingi kupita aina nyingine zote za madini yanayopatikana nchini.

Akizungumza na wafanyakazi wa Ofisi ya Madini Dodoma, Machi 22 mwaka huu akiwa kwenye ziara ya kazi, Biteko alisema kuwa takwimu za makusanyo ya Serikali zinabainisha hayo.

“Mfano mwaka 2016/17, takribani tani milioni 15.6 za madini ya ujenzi zilizochimbwa, zilizalisha shilingi bilioni 230.6; ambapo katika hiyo, ulipatikana mrabaha wa shilingi bilioni 7.1,” alisema.

Akifafanua zaidi, Naibu Waziri Biteko alieleza kuwa, idadi ya wachimbaji wa dhahabu na madini mengine nchi nzima ikijumlishwa, haiwezi kufika hata robo ya wale wanaofanya shughuli za madini ya ujenzi nchini.

Alisema kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha inaongeza vituo vya madini ya ujenzi na viwanda kutoka 85 vilivyopo sasa nchi nzima hadi kufikia 174. “Nina uhakika tukiviongeza vituo kufikia idadi hiyo, tutakusanya mrabaha wa zaidi ya shilingi bilioni 15 katika madini hayo pekee.”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...