NAIBU
Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira,
Mhe. Antony Mavunde amekitoza faini ya shilinhgi milioni 35 (milioni
thelathini na tano), kiwanda cha kusokota nyuzi cha PPTL kilichoko eneo
la Kange Mkoani Kilimanjaro.
Mhe. Mavunde alichukua uamuzi huo, wakati wa ziara yake ya kushtukiza aliyoifanya Mkoani humo Machi 2, 2018 ili kubaini waajiri ambao hawatekeelzi inavyopasa Sheria ya ajira na mahusiano kazini na wale ambao bado hawajajisajili na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF).
Naibu Waziri Mavunde, alikuta wafanyakazi wa kiwanda hicho ambacho kina mashine nyingi na kutokana na mfumo wa utendaji kazi wake, kinatoa kelelenyingi hawakuvaa vifaa vya kujikinga na madhara kazini, (protective gears).
Mhe. Mavunde aliwakuta baadhi yao wakiwa wamevaa kandambiloi, wengine hawana vifaa vya kuziba masikio kujihami na kelele, pamoja na vifaa vingine. Hatua hiyo ilimkasirisha Mhe. Navu Waziri na kumuagiza Afisa wa OSHA, kuchukua hatua mara moja ambapo kiwanda hicho kilitozwa faini ya shilingi milioni 35 kwa kukiuka Sheria ya ajira na mahusiano kazini ambapo pamoja na mambo mengine inasisitioza usalama mahala pa kazi kwa wafanyakazi kuvaa vifaa vya kujihami.
Aidha Mhe. Mavunde ambaye kabla ya kufika Mkoani Tanga, alitembelea mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Kilimanjaro, ameuagiza uongozi wa kiwanda hivho kuondoa kasoro hizo mara moja.Sambamba na hilo, Mhe. Mavunde amesema, serikali haitabadili msimamo wake wa kuwafikisha mahakamani waajiri wote ambao bado hawajatekeelza takwa la kisheria la kujisajili na kupeleka michango kwenye Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF) kwani kwa kutofanya hivyo wanakabiliwa na adhabu mbalimbali ikiwemo kupelekwa mahakamani ambapo mwajiri atakayepatikana na hatia atalazimika kulipa faini ya kiasi kisichopungua Shilingi Milioni 50,000, (Milioni Hamsini), au kifungo kisichopungua miaka mitano (5) au vyote kwa pamoja.
Mhe. Mavunde alichukua uamuzi huo, wakati wa ziara yake ya kushtukiza aliyoifanya Mkoani humo Machi 2, 2018 ili kubaini waajiri ambao hawatekeelzi inavyopasa Sheria ya ajira na mahusiano kazini na wale ambao bado hawajajisajili na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF).
Naibu Waziri Mavunde, alikuta wafanyakazi wa kiwanda hicho ambacho kina mashine nyingi na kutokana na mfumo wa utendaji kazi wake, kinatoa kelelenyingi hawakuvaa vifaa vya kujikinga na madhara kazini, (protective gears).
Mhe. Mavunde aliwakuta baadhi yao wakiwa wamevaa kandambiloi, wengine hawana vifaa vya kuziba masikio kujihami na kelele, pamoja na vifaa vingine. Hatua hiyo ilimkasirisha Mhe. Navu Waziri na kumuagiza Afisa wa OSHA, kuchukua hatua mara moja ambapo kiwanda hicho kilitozwa faini ya shilingi milioni 35 kwa kukiuka Sheria ya ajira na mahusiano kazini ambapo pamoja na mambo mengine inasisitioza usalama mahala pa kazi kwa wafanyakazi kuvaa vifaa vya kujihami.
Aidha Mhe. Mavunde ambaye kabla ya kufika Mkoani Tanga, alitembelea mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Kilimanjaro, ameuagiza uongozi wa kiwanda hivho kuondoa kasoro hizo mara moja.Sambamba na hilo, Mhe. Mavunde amesema, serikali haitabadili msimamo wake wa kuwafikisha mahakamani waajiri wote ambao bado hawajatekeelza takwa la kisheria la kujisajili na kupeleka michango kwenye Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF) kwani kwa kutofanya hivyo wanakabiliwa na adhabu mbalimbali ikiwemo kupelekwa mahakamani ambapo mwajiri atakayepatikana na hatia atalazimika kulipa faini ya kiasi kisichopungua Shilingi Milioni 50,000, (Milioni Hamsini), au kifungo kisichopungua miaka mitano (5) au vyote kwa pamoja.
Naibu Waziri akitembelea kiwanda hicho.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde,(watatu kulia), akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda cha kusokota nyuzi cha PPTL kilichoko Kange Mkoani Tanga, baada ya kuwakuta wakifanya kazi bila ya kuwa na vifaa vya kujikinga, (protrctive gears), alipofanya ziara ya kushtukiza kiwandani hapo ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kuwabaini waajiri ambao hawatekelezi sharia ya kazi na mahusiano kazini sambamba na kuwabaini waajiri a,mbao hawajajisajili na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi (WCF) Mkoani humo Machi 2, 2018.
Nabu Waziri Mavunde, akiwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa WCF, Bw. Anselim Peter, wakati walipotembelea kiwanda bhicho cha PPTL.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...