Na Ripota Wetu,Globu ya Jamii

MEYA  wa Jiji la Dar es Salaam , Isaya Mwita ametemtembelea nyumbani kwakwe na kisha kumpeleka katika Hospitali ya Taifa Muhimbili mwasisi na mkongwe wa Chadema Victa Kimesela ambaye anaumwa kwa muda mrefu sasa.

Kimesela ni miongoni mwa waasisi walioshiriki kuandaa Katiba ya chama hicho mwaka 1992, anaugua kwa muda ambapo familia yake ilimueleza Meya Mwita kuwa alilazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na hivyo kuruhusiwa Jumatano iliyopita.

Taarifa iliyotolewa leo na Ofisa Habari wa Ofisi ya Meya wa Jiji la Dar es Salaam Christina Mwagala amesema muda fupi baada ya  Meya Mwita kufika nyumbani  kwa mwasisi huyo, afya yake ilibadilika.

Hivyo kwa kushirikiana na familia hiyo  walitoa taarifa Muhimbili ili kupatiwa gari ya kubebea wa gonjwa.Aidha  gari hiyo ilifika na kisha Mwita na familia hiyo waliambatana pamoja kumuwahisha kwa mara nyingine Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo alikuwa akipatiwa matibabu awali.

 Mwagala amesema kuwa Kimesela amewahi kushika nafasi mbalimbali ndani ya Chadema, ikiwepo kuwa Katibu mtendaji wa chama hicho wakati wa utawala wa mzee Edwin Mtei.

Pia amewahi kuwa Katibu mkuu wa muda wakati wa utawala wa Bob Makani(marehemu)na hivyo kumuachia nafasi hiyo Dk.Wilblod Slaa ambaye kwa sasa amestaafu siasa tangu  mwaka 2015.
 
Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam , Isaya Mwita akiwa pamoja na familia ya Kimesela ,wakitoa msaada wa kumpakiza kwenye gari ya kubebea wagonjwa ya hospital ya Taifa Muhimbili jana alipomtembelea nyumbani kwakwe.Kimesela anaumwa na kwa sasa amelazwa katika hospital ya Taifa Muhimbili.
Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akizungumza na mke wa Kimesela , Suzani Kimesela alipomtembekea nyumbani kwake jana .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...