Wananchi wa mtaa wa Tungwi-Songani Kata ya Pembamnazi Manispaa ya Kigamboni wametakiwa kutunza miundombinu ya soko ili soko liweze kudumu kwa muda mrefu na kunufaisha wananchi wote kwa ujumla. 

Rai hiyo imetolewa jana na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mh.Maabadi Hoja alipokuwa akizindua mradi wa soko hilo ijumaa lililojengwa Mtaa wa Tundwi-Songani , alisema kuwa mradi huu umenza ujenzi muda mrefu tangu mwaka 2002, hivyo tunatarajia ukamilikaji wake utaleta maendeleo kwa wananchi wote wa Tundwi Songani na jamii nzima ya Kata ya PembaMnazi hivyo ni muhimu kuhakikisha unatunzwa. 

Alisema kuwa ulinzi uimarishwe wa miundombinu na kuhakikisha lengo lililokusudiwa la kuboresha mazingira na utoaji wa huduma kwa wafanyabiashara na wananchi wa Tundwi na kata ya Pemba Mnazi kwa ujumla linafikiwa. 

Akitoa taarifa ya mradi Mratibu wa TASAF Manispaa ya kigamboni Bi.Janet Kacholi alisema kuwa, mradi wa soko ni miongoni mwa miradi iliyoibuliwa na wananchi kupitia program ya TASAF, ambapo umelenga kutoa ajira kwa vijana kwa kupata fursa ya kuuza mazao mbalimbali na kuiwezesha Serikali kupitia Halmashauri kukusanya mapato kutokana na ushuru mbalimbali utakaotozwa kwa wafanyabiashara. 

Aliongeza kuwa hadi kukamilika kwa ujenzi wa soko hilo jumla ya Tsh.91,858,842.24 zimetumika ambapo wananchi wamechanga kiasi cha Tsh.34.040.427.27 mchango wa TASAF ni Tsh.26,416,827.27 na Halmashauri ya Manispa ya kigamboni imetoa Tsh.31,401,587.7 ambazo zimekamilisha ujenzi wa meza za ndani baada ya Halmshauri ya Temeke kushindwa kutoa fedha za ukamilishaji kama ilivyoahidi wakati wa uibuaji wa mradi kabla ya kugawanywa. 
 ​Mstahiki Meya wa Manispaa ya kigamboni Mh. Maabadi Hoja akifungua kitambaa cha jiwe la msingi kuonesha uzinduzi rasmi wa soko​


 ​Mratibu wa TASAF Manispaa ya Kigamboni Bi. Janet Kacholi akisoma taarifa ya mradi kabla ya uzinduzi.​
 ​Mstahiki Meya akiwa ameongozana na wananchi wakikagua soko mara baada ya uzinduzi. 


 ​muonekano wa soko kwa nje​
 ​Baadhi ya wananchi walioshiriki uzinduzi wa soko​.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...