Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theoblad Sabi (kushoto), akizungumza na
waandishi wa habari kabla hajakabidhi zawadi ya gari aina ya Suzuki Carry ‘kirikuu’
yenye thamani za zaidia ya shs miliono 30 kwa mshindi wa kampeni ya Malengo ya
NBC, Fatuma Saidi Ramadhani (kulia). Alisema moja na malengo la kapeni hiyo ni
kuhamasisha wateja na wasio wateja kujiwekea akiba katika benki hiyo ili
kutimiza malengo.
Mshindi wa zawadi ya gari ya kampeni ya
Malengo ya NBC, Fatuma Saidi Ramadhani akihojiwa na waandishi wa vyombo
mbalimbali vya habari katika hafla hiyo.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kushoto), akikabidhi kadi ya gari aina ya Suzuki Carry
‘kirikuu’ kwa Fatuma Saidi
Ramadhani, mmoja wa washindi
sita wa kampeni ya Malengo ya NBC
jijini Dar es Salaam jana. Anayeangalia ni Mkurugemnzi wa Wateja Binafsi wa
benki hiyo, Filbert Mponzi. Kampeni hiyo ilidumu wa muda wa miezi mitatu.
Mshindi wa zawadi ya gari ya kampeni yas
Malengo ya NBC, Fatuma Saidi Ramadhani (katikati), akionyesha kadi ya gari lake
baada ya kukabidhiwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi
(kushoto). Kulia ni Mkurugenzi wa Wateja
Binafsi wa benki hiyo, Filbert Mponzi na baadhi ya familia ya mshindi huyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...