Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Kippi Warioba(Wa Pili kutoka kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Malipo ya Ankara za Maji kwa njia ya NMB Mobile leo,uzinduzi ulioenda sambamba na uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Maji kwa mkoa wa Kilimanjaro.Wengine toka kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Michael Mwandezi,Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi(MUWSA) Joyce Msiru,akifuatiwa na Meneja wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela ,Emanuel Kishosha.
 Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba akizungumza wakati wa uzinduzi wa Maadhimisho ya wiki ya Maji mkoa wa Kilimanjaro,uzinduzi uliifanyika leo katika viwanja jirani na ofisi za MUWSA.
 Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,(MUWSA) Joyce Msiru akitoa taarifa juu ya utoaji wa Huduma ya Maji kwa mgeni rasmi ,Kippi Warioba katika uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Maji mkoa wa Kilimanjaro.
Meneja wa Benki ya NMB tawi la Nelson Emanuel Kishosha akitoa maelezo kwa mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba wakati wa maadhimisho ya wiki ya Maji mkoa wa Kilimanjaro yaliyoenda sambamba na uzinduzi wa malipo ya Ankara za Maji kwa njia ya NMB Mobile.
 Meneja wa Benki ya NMB tawi la Nelson Emanuel Kishosha akitoa maelezo kwa mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba wakati wa maadhimisho ya wiki ya Maji mkoa wa Kilimanjaro yaliyoenda sambamba na uzinduzi wa malipo ya Ankara za Maji kwa njia ya NMB Mobile.
 Mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru akiotesha Mti katika eneo la chanzo cha Maji cha Kaloleni.Jumla ya ya miti 500/imeoteshwa katika eneo hilo ikiwa ni msaada uliotolewa na taasisi ya Kilimanjaro Project.
 Mgeni rasmi katika uzinduzi wa Maadhimisho ya wiki ya Maji mkoa wa Kilimanjaro, Mkuu wa Wilaya ya Moshi,Kippi Warioba akiotesha mti katika eneo la chanzo cha Maji cha Kaloleni Mara baada ya kuzindua wiki ya Maji mkoa wa Kilimanjaro ikibeba kauli mbiu ya "hifadhi maji na mfumo Wa kiikologia kwa maendeleo ya jamii"
 Mgeni rasmi katika Uzinduzi wa Maadhimisho ya wiki ya Maji ,Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba akikagua baadhi ya mabanda ya maonesho yaliyopo katika viwanja vilivyopo jirani na ofisi za MUWSA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...