SERIKALI ya Mkoani Tabora imesema kuanzia msimu ujao mazao yote ni lazima yalimwe kwa kuzingatia kanuni za kilimo bora kinachosisitiza matumizi ya mbolea na ujazaji wa mazao kitaaalamu ili kuhakikisha kunakuwa na mavuno mengi ambayo yatawawezesha wakulima kuzalisha ziada ambayo itawasaidia kuwaletea maendeleo yao binafsi.
Kauli hiyo ilitolewa jana Wilayani Kaliua na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati akiendelea na kampeni zake za kuelimisha wakulima wa pamba juu ya matumizi sahihi ya dawa za kuua wadudu waharibifu katika pamba.
Alisema ulimaji wa hivi sasa kwa wakulima walio wengi hauzingatii ujazaji wa miche(plant population) kitaalamu katika mashamba yao na matumizi ya mbolea jambo linalopelekea kuwepo na mavuno machache katika eneo kubwa shamba hatua ambayo inamfanya mkulima kuwa na mavuno machache.
Kufuatia hatua hiyo Mkuu huyo wa Mkoa alisema kilimo kijacho ni lazima wakulima wote waliopo Mkoani Tabora walime kilimo kinachowasaidia kuzalisha ziada na kupata fedha kwa ajili ya kupanua kilimo chake na kuboresha maisha yao.
"Kuanzia sasa ni marufuku kwa wakulima kwa Mkoa huu kulima zao lolote iwe mchicha, viazi , mahindi na mazao ya biashara bila kufuata mistari na kujaza mazao katika shamba...siwezi kuendelea kuvumilia wakulima wanaendelea kulima kilimo ambacho hakiwasaidia kupiga hatua na kuondokana na umaskini kwa kuzalisha mazao mengi katika eneo dogo" alisema Mkuu huyo wa Mkoa.
Katibu
Tawala Wilaya ya Kaliua Michael Nyahinga( wa pili kutoka kushoto)
akitoa maelezo jana kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri( wa pili
kulia) wakati alipotembelea shamba la pamba la Mkuu wa Wilaya ya Kaliua
Abel Busalama ikiwa ni sehemu ya kuwaelimisha wakulima wa zao juu ya
matumizi sahihi ya dawa za kuua wadudu. Wengine ni Mratibu wa Pamba wa
Wilaya ya Kaliua Samwel Mushi(kushoto) na Mshauri wa Kilimo kutoka Ofisi
ya Mkuu wa Mkoa Modest Kaijage(kulia).
Mshauri
wa Kilimo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Modest Kaijage(kulia) akitoa
maelezo jana kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri( wa pili kulia)
wakati alipotembelea shamba la pamba la Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Abel
Busalama ikiwa ni sehemu ya kuwaelimisha wakulima wa zao juu ya matumizi
sahihi ya dawa za kuua wadudu. Wengine ni Katibu Tawala Wilaya ya
Kaliua Michael Nyahinga(kushoto) na Afisa Tarafa ya Kaliua Bethod
Mahenge (wa pili kulia)
Mkuu
wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri(wa pili kushoto) akizungumza jambo jana
kwa Katibu Tawala Wilaya ya Kaliua Michael Nyahinga( kushoto) wakati
alipotembelea shamba la pamba la Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Abel Busalama
ikiwa ni sehemu ya kuwaelimisha wakulima wa zao juu ya matumizi sahihi
ya dawa za kuua wadudu. Wengine ni Afisa Tarafa ya Kaliua Bethod
Mahenge(wa pili kulia) na Mshauri wa Kilimo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa
Tabora Modest Kaijage(kushoto). Picha na Tiganya
Vincent
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...