Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani,Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mjini Shinyanga (SHUWASA) imeendesha semina kwa wanawake wa manispaa ya Shinyanga kuwapa elimu kuhusu utoaji huduma ya maji safi na usafi wa mazingira.
Mgeni rasmi katika semina hiyo iliyofanyika leo (jana) Jumatano Machi 7,2018 katika ukumbi wa Shinyanga Vijana Centre Mjini Shinyanga alikuwa Mkuu wa wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro.
Akifungua semina hiyo,Matiro aliushukuru uongozi wa SHUWASA kwa kuthamini umuhimu wa akina mama katika jamii akieleza kuwa akina mama ni muhimili mkubwa katika malezi ya familia na jamii lakini pia ndiyo walengwa wakubwa wa huduma ya maji katika maisha ya kila siku.
"Kwa kuzingatia kauli mbiu ya kitaifa ya mwaka huu inayosema 'Kuelekea uchumi wa viwanda: Tuimarishe usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake vijijini',ni dhahiri kuwa taifa limetambua nafasi ya mwanamke katika jamii,SHUWASA nawashukuru kwa kuwapa kipaumbele akinamama katika uendelezaji na usimamizi wa mipango na mikakati ya huduma ya maji safi",alisema.
"Akina mama ni nguzo muhimu sana katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto za maji kwani huduma ikiwa dhaifu,waathirika wakubwa wa hali hiyo ni akina mama na watoto hivyo ni vyema wadau wote tukashirikiana kutatua changamoto zinazojitokeza",aliongeza Matiro.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akifungua semina ya wanawake wa Manispaa ya Shinyanga iliyoandaliwa na SHUWASA kama moja ya matukio ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Akina mama wa Manispaa ya Shinyanga wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.
Makamu mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi SHUWASA, Joyce Egina akizungumza wakati wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa semina hiyo, Ziphora Pangani (Mkuu wa wilaya mstaafu) akiongoza kipindi cha majadiliano wakati wa semina.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...