KAIMU Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Ernest Mkongo amefunga Mafunzo Elekezi ya kubaini watoto wenye mahitaji maalum yaliyowahusisha wataalam watambuzi hao mjini Morogoro.

Akitoa hotuba yake, mbele ya walimu, maafisa ustawi wa Jamii na baadhi ya madaktari, Mkongo amesema ana imani kubwa na wataalamu hao ambao wamepatiwa mafunzo ya kubaini kwa kutumia vifaa maalum kuwa watafikia malengo ya kazi waliyoelekezwa na Serikali ili kuboresha huduma ya elimu bora kwa watoto wenye mahitaji maalum nchini.

“Ni matumaini yangu baada ya mafunzo haya kuwa kila mmoja wenu atakuwa na ujuzi wa
kutosha kutumia vifaa maalum kuwabaini watoto wenye changamoto za uoni hafifu, ujongeaji wa viungo vya mwili, usikivu, changamoto nyingine ambazo hutegemea hali ya afya na mazingira,”Amesema.

Amesema Watoto hao wanatarajiwa kutoka rika la miaka minne hadi sita na kwamba wataalam hao watatoa ushauri wa kitaalam na kitabibu kwa wazazi na walezi wa watoto hao, na walimu wa watoto watakaobainika hivyo ni vema wakaifanya kazi hiyo kwa umakini na weledi mkubwa ili malengo ya Serikali yatimie.
 Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Ernest Mkongo akifunga Mafunzo Elekezi ya kubaini watoto wenye mahitaji maalum yaliyowahusisha wataalam watambuzi hao mjini Morogoro.
 Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Elimu (Elimu ya Watu Wazima), Ofisi ya Rais TAMISEMI, Kassim Kaoneka akitoa neno la awali kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi. 
 Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Ernest Mkongo (kushoto) akiteta jambo na Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Elimu (Elimu ya Watu Wazima), Ofisi ya Rais TAMISEMI, Kassim Kaoneka.
Baadhi ya washiriki wa Mafunzo Elekezi ya kubaini watoto wenye mahitaji maalum yaliyowahusisha wataalam watambuzi hao mjini Morogoro.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...