KAIMU Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Ernest Mkongo
amefunga Mafunzo Elekezi ya kubaini watoto wenye mahitaji maalum yaliyowahusisha
wataalam watambuzi hao mjini Morogoro.
Akitoa hotuba yake, mbele ya walimu, maafisa ustawi
wa Jamii na baadhi ya madaktari, Mkongo amesema ana imani kubwa na wataalamu
hao ambao wamepatiwa mafunzo ya kubaini kwa kutumia vifaa maalum kuwa watafikia
malengo ya kazi waliyoelekezwa na Serikali ili kuboresha huduma ya elimu bora
kwa watoto wenye mahitaji maalum nchini.
“Ni matumaini yangu baada ya mafunzo haya kuwa kila
mmoja wenu atakuwa na ujuzi wa
kutosha kutumia vifaa maalum kuwabaini watoto wenye
changamoto za uoni hafifu, ujongeaji wa viungo vya mwili, usikivu, changamoto
nyingine ambazo hutegemea hali ya afya na mazingira,”Amesema.
Amesema Watoto hao wanatarajiwa kutoka rika la
miaka minne hadi sita na kwamba wataalam hao watatoa ushauri wa kitaalam na
kitabibu kwa wazazi na walezi wa watoto hao, na walimu wa watoto watakaobainika
hivyo ni vema wakaifanya kazi hiyo kwa umakini na weledi mkubwa ili malengo ya
Serikali yatimie.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Ernest Mkongo akifunga
Mafunzo Elekezi ya kubaini watoto wenye mahitaji maalum yaliyowahusisha
wataalam watambuzi hao mjini Morogoro.
Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Elimu (Elimu ya Watu Wazima),
Ofisi ya Rais TAMISEMI, Kassim Kaoneka akitoa neno la awali kabla ya kumkaribisha
mgeni rasmi.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Ernest Mkongo (kushoto)
akiteta jambo na Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Elimu (Elimu ya Watu
Wazima), Ofisi ya Rais TAMISEMI, Kassim Kaoneka.
Baadhi ya washiriki wa Mafunzo Elekezi ya kubaini watoto
wenye mahitaji maalum yaliyowahusisha wataalam watambuzi hao
mjini Morogoro.KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...