*Rais Chama cha Madaktari bingwa wa figo atoa sababu, atoa ushauri kwa Watanzania

Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii

CHAMA cha Madaktari Bingwa wa magonjwa ya figo Tanzania kimepiga marufuku biashara  ya uuzaji figo nchini na kueleza kuwa huo si utaratibu mzuri kwa madhara yake ni makubwa.

Pia kimeelezea hali ya ugonjwa wa figo nchini na kwamba kwa mwaka huu wanatarajia kupandikiza figo kwa wagonjwa 50 huku kikielezea jitihada za Serikali katika kuhamasisha wananchi kuzuia ugonjwa figo.

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Rais wa Chama cha Madaktari bingwa ya figo Tanzania Dk.Onesmo Kisanga wakati anazungumza na Michuzi Blogu,ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Figo Duniani ambayo huadhimishwa kila Alhamis ya pili ya kila Machi.Siku hiyo hutumika kutoa elimu kuhusu ugonjwa wa figo na hatua ambazo wanataalamu wanachukua ili kukabiliana nao.

Akizungumzia kuhusu tabia ya watu kuuza figo ili kupata fedha,Dk.Kisanga ambaye pia ni Daktari bingwa wa magonjwa ya figo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili amesema kuwa kwa sasa wamepiga marufuku biashara ya watu kuuza figo kwani ina madhara makubwa.

“Nikiri tunapokea maombi mengi pale Muhimbili kutoka kwa watu ambao wanataka kuuza figo ili wapate fedha.Nieleze tu hii biashara ya kuuza figo haitakiwi kabisa nchini Tanzania.Hata Chama cha madaktari bingwa duniani nacho kimepiga marufuku biashara ya figo,"amesema Dk.Kisanga.

Amesema kikubwa ambacho wanakifanya ni kuendelea kutoa elimu kwa wale ambao wanataka kuuza figo kuwa hairuhusiwi na kubwa zaidi ikifanywa ni biashara maana yake wale wasiokuwa na uwezo watashindwa kununua matokeo yake watokosa matibabu.

WATU 50 KUPANDAKIZWA FIGO MWAKA HUU
Wakati huo huo Dk.Kisanga amesema mwaka huu wanatarajia kupandikiza figo kwa wagonjwa 50 na huo ndio mkakati wao na kufafanua kuwa mwezi huu wanatarajia kupandikiza figo kwa wagonjwa watano na mwezi unaokuna watapandikiza kwa wagonjwa saba.Serikali ya Awamu ya Tano imeamua kutoa kipaumbele kwenye sekta ya afya na hivyo kufanya idadi ya madaktari bingwa katika kutibu magonjwa ya figo kuongezeka.
"Kwa mara ya kwanza Tanzania tulipandikiza figo mwaka 2017 na tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa.Aliyepandikizwa figo yupo salama na aliyetoa figo naye yupo salama,"amesema Dk.Kisanga.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Nakubaliana na daktari kwamba uuzaji ya figo ama jicho au meno haupendezi.Lakini nikitaka kujitolea kumpa mtu figo langu
    moja naruhusiwa.So what is unpleasant is the exchange of money. Je nikimpa mtu figo naye akinipa nyumba inaruhusiwa? All over the world hundreds of people are dying everyday waiting for free donors,just think for a moment if the sale of kidneys were allowed,would there be these unnecessary daily deaths? We just have this thing that selling a kidney is wrong, but......just stop and think of all other tradings going on. We are allowed to sell poisons,alcohol, tobacco and guns...........If I were hungry and I have money, think how I would feel if I were told that I could not buy food, I have to wait for free food donation or die, I know its a silly example but I hope you get my point.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...