Meneja Mawasiliano wa Halotel, Hindu Kanyamala (Kulia) pamoja na Meneja
wa mahusiano wa Halotel Stella Pius kwa pamoja wakiongea na wananchi
katika soko la makumbusho, Dar es Salaam, jana ,kuhusu kampeni yao mpya
ya kununua bando kwa Halopesa ambapo mamilioni ya wateja kunufaika kwa
kupata huduma za mawasiliano kwa bei nafuu Zaidi, ikiwa ni muendelezo
wa kampeni yao ya kufikia mteja mmoja mmoja .
Katika
kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia ya mawasiliano nchini, Kampuni
ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Halotel imeendelea kubuni mbinu
mpya kuhakikisha kwamba wateja wake wa kada zote wanapata suluhisho la
changamoto ya gharama za mawasiliano na kupata huduma hii kwa urahisi
zaidi.
Ikiwa ni mkakati wa kuendelea kuboresha huduma, Halotel, Imepunguza gharama za mawasiliano kwa wateja wake kwa kuzindua huduma mpya ya Nunua Vifurushi maalum kwa Halopesa ili kuwawezesha wateja wa mtandao huo kuepuka gharama kubwa za mawasiliano.
Akizungumza katika uzinduzi wa huduma hiyo, Naibu Mkurugenzi wa kampuni hiyo Bwana Nguyen Van Son, amesema kuwa huduma hiyo itawawezesha wateja wote nchi nzima kuweza kununua vifurushi maalum kupitia Halopesa ambapo wamezingatia uhitaji wa mahitaji yao
“Huduma hii inawalenga wateja wa vipato vya chini wanaofanya mawasiliano yanayolingana na wenye vipato vya kati lakini wanapata huduma hii kwa gharama nafuu kwa kujiunga kupitia Halopesa tofauti na wateja wengine, aliongeza Son”.
Mfano; kwa mteja anayetumia shilingi mia tano (500) kwa siku, kwa sasa anaweza kujiunga na kifurushi hiki maalum kupitia Halopesa akapata hadi dakika 32 za kupiga simu mitandao yote, Mb 250 za intaneti na ujumbe mfupi (SMS) 550, vilevile kwa shilingi mia tano (500)hiyohiyo mteja anaweza kujiunga na kifushi cha wiki akapata Mb 300 za intaneti za kutumia kwa wiki nzima.
Hatuishi
hapo, kwa mteja anayetumia shilingi elfu moja ( 1000) anaweza kujiunga
na kupata hadi dakika 52 za kupiga mitandao yote, Mb 350 za intaneti na
ujumbe mfupi (SMS) 1000 za kutumia kwa wiki nzima kujiunga kupitia
Halopesa kupiga code namba *150*88# na kuchagua namba 2. ” Alisema Son.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...