Meneja Mawasiliano wa Halotel, Hindu Kanyamala (Kulia) pamoja na Meneja wa mahusiano  wa Halotel Stella Pius kwa pamoja  wakiongea na wananchi katika soko la makumbusho, Dar es Salaam, jana ,kuhusu  kampeni yao mpya ya kununua bando kwa Halopesa  ambapo mamilioni ya wateja kunufaika kwa kupata huduma za mawasiliano kwa bei nafuu Zaidi, ikiwa ni muendelezo wa kampeni yao ya kufikia mteja mmoja mmoja . 
 Katika kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia ya mawasiliano nchini, Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Halotel imeendelea kubuni mbinu mpya kuhakikisha kwamba wateja wake wa kada zote wanapata suluhisho la changamoto ya gharama za mawasiliano na kupata huduma hii kwa urahisi zaidi.

Ikiwa ni mkakati wa kuendelea kuboresha huduma, Halotel, Imepunguza gharama za mawasiliano kwa wateja wake kwa kuzindua huduma mpya ya Nunua Vifurushi maalum kwa Halopesa ili kuwawezesha wateja wa mtandao huo kuepuka gharama kubwa za mawasiliano.

Akizungumza katika uzinduzi wa huduma hiyo, Naibu Mkurugenzi wa kampuni hiyo Bwana Nguyen Van Son, amesema kuwa huduma hiyo itawawezesha wateja wote nchi nzima kuweza kununua vifurushi maalum kupitia Halopesa ambapo wamezingatia uhitaji wa mahitaji yao

“Huduma hii inawalenga wateja wa vipato vya chini wanaofanya mawasiliano yanayolingana na wenye vipato vya kati lakini wanapata huduma hii kwa gharama nafuu kwa kujiunga kupitia Halopesa tofauti na wateja wengine, aliongeza Son”.

Mfano; kwa mteja anayetumia shilingi mia tano (500) kwa siku, kwa sasa anaweza kujiunga na kifurushi hiki maalum kupitia Halopesa akapata hadi dakika 32 za kupiga simu mitandao yote, Mb 250 za intaneti na ujumbe mfupi (SMS) 550, vilevile kwa shilingi mia tano (500)hiyohiyo mteja anaweza kujiunga na kifushi cha wiki akapata Mb 300 za intaneti za kutumia kwa wiki nzima. 
Hatuishi hapo, kwa mteja anayetumia shilingi elfu moja ( 1000) anaweza kujiunga na kupata hadi dakika 52 za kupiga mitandao yote, Mb 350 za intaneti na ujumbe mfupi (SMS) 1000 za kutumia kwa wiki nzima kujiunga kupitia Halopesa kupiga code namba *150*88# na kuchagua namba 2. ” Alisema Son.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...