Katika kijiji cha EWORENDEKE, kata ya KIMOKOUWA, Wilayani LONGIDO mkoani ARUSHA, kijiji hicho kipo takriban kilomita 4 kutoka Namanga, mpaka wa Tanzania na Kenya.

Hapo kuna Soko la Kimkakati la mifugo Longido, linalohusika na uuzaji wa mifugo kutoka mikoa takribani 7 ya hapa nchini Tanzania. Wafugaji huuza mifugo hiyo hapa nchini na nchi za jirani, soko hilo ambalo limejengwa na Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF), limekuwa ni neema kwa watoto wa kaya zinazozunguka soko hilo.

Watoto wa wafugaji wa jamii ya kimaasai ambao ndiyo wanufaika wa soko hilo wameguswa na uwepo wa soko hilo kwa kupata maziwa ya mbuzi bure. Watoto hao hukamua maziwa hayo kutoka kwa mbuzi ambao hufikishwa sokoni hapo muda wa jioni na kusubiri kuuzwa usiku ambapo mnada wa mifugo kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi hufanyika sokoni hapo.

Mratibu wa Kitaifa wa Program ya MIVARF,Walter Swai, amebainisha kuwa tangu Program hiyo ianzishwe kutekelezwa rasmi mwaka 2011, katika mikoa yote ya Tanzania bara na Zanzibar imekuwa ikichochea faida nyingi, zaidi ya malengo mahususi yaliyokusudiwa na Program ambayo, ni kufanikisha azma ya Serikali ya Tanzania ya kuongeza kipato kwa wananchi pamoja na uhakika wa chakula kwa kaya zenye kipato cha chini hususan maeneo ya vijijini.
 Baadhi ya watoto wa wafugaji, kijiji cha Eworendeke, kata ya Kimokouwa, Wilayani Longido wakipata maziwa kwa ajili ya matumizi yao kwa kukamua bure mbuzi waliofikishwa muda wa jioni katika Soko la kimkakati la mifugo Longido kuuzwa, Soko hilo limejengwa na Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).
 Mmoja wa watoto wa wafugaji, kijiji cha Eworendeke, kata ya Kimokouwa, Wilayani Longido akipata maziwa kwa ajili ya matumizi yake kwa kukamua bure mbuzi waliofikishwa muda wa jioni katika Soko la kimkakati la mifugo Longido kuuzwa, Soko hilo, limejengwa na Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...