Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga imesema mpaka ifikapo machi 31 mwaka huu, itawachukulia hatua Kali za kisheria wazazi na walezi wote ambao watoto wao wamefaulu na hawajaripoti shuleni mpaka sasa kwa Sababu zisizo na msingi. 

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu Wa wilaya ya Mkuranga wakati akifungua kikao cha bajeti ya mwaka 2018/2019 cha baraza la madiwani kilicho fanyika wilayani humo,na kusema kuwa wanafunzi walioripoti ni 3,439 sawa na asilimia 46 na wanafunzi 217 hawajaripoti mpaka sasa ambao ni sawa na asilimia 5.46.

Aidha amesema mpaka ifikapo march 31 mwaka huu,wazazi na walezi ambao watakuwa hawajatoa taarifa zozote kuhusu sababu za watoto wao kutoripoti shuleni watachukuliwa hatua Kali za kisheria.

Aidha Sanga amewataka madiwani wote  wa wilaya hiyo kushirikiana nae kufuatilia kwa undani suala hilo ili kuhakikisha kuwa wanabaini changamoto zilizopelekea wanafunzi hao kutofika shuleni mpaka sasa."tunachotaka watoto wetu wasome,hatutaki kusukia mtu ameacha shule kwasababu ya kuolewa,wazazi watoe taarifa vinginevyo hatua zitachukuliwa dhidi yao".alisema Sanga.
Mwenyekiti Wa Halmashauri ya Mkuranga,Juma Abeid akizungumza na Madiwani wa Wilaya ya Mkuranga katika mkutano wa bajeti ya mwaka 2018/2019.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
Diwani wa kata ya Mwanandege,Adroph Kowero akifafanua jambo katika mkutano huo.
Madiwani wakimsikiliza Mwenyekiti Wa Halmashauri ya Mkuranga,Juma Abeid.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...