Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii.
RAIS wa Marekani Donald Trump ameeleza mpango wake wa kupambana na wauzaji wa dawa za kulevya chini humo.
Akihutubia huko Manchester, Trump amesema kuwa dawa za kulevya yanagharimu maisha ya watu wengi kutokana na matumizi ya dawa na wanaosababisha vifo hivyo hupewa adhabu ya muda mfupi.
Amefafanua na tayari Bunge limetenga kiasi cha dola za Marekani bilioni sita kwa ajili ya kupambana na tatizo hilo.
Ameeleza lazima kuwe na umakini na kuelekeza adhabu kali sambamba na ile ya kifo kwa wauzaji wa madawa ya kulevya.
Ifahamike katika kampeni zake za urais Trump alitoa ahadi nzito zikiwemo kujenga ukuta ili kudhibiti wahamiaji haramu, kutengua mpango wa afya wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Obama Barrack na ile ya Marekani kwanza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...