Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
KUELEKEA uchumi wa viwanda kampuni ya usambaaji  mbolea ya Yara Tanzania imepunguza gharama Mbolea YaraMila Otesha kwa asilimia 50 ili kuwezesha wakulima wazalishe mazao  bora yatayongia katika viwanda  vya bidhaa mbalimbali.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Meneja Masoko wa Kampuni hiyo, Linda Byaba amesema kupunguza bei ya mbolea kwa asilimia 50  ni kuwawezesha wakulima waweze kumudu gharama hizo.

Amesema Yara ni kampuni inayoongoza duniani kwa uzalishaji wa mbolea zenye virutubisho linganifu kama YaraMila. Kila punje moja ya YaraMila ina virutubisho vyote kama Nitrojeni, Fosiforasi, Kalisiam, Boroni, Magniziam kwa ajili ya kuupa mmea lishe linganifu.

Byaba amesema wakulima wanaozalisha mazao ya nafaka, kahawa, chai, sukari, tumbaku, alizeti, viazi na mbogamboga wanafaidika na mbolea zenye virutubisho kupitia matawi yake yaliyopo Tanzania na Rwanda.

Amesema faida za mbolea hii ya Kupandia ya YaraMila Otesha , lishe linganifu ya mmea ,ni mbolea ya NPK yenye kiwango cha juu cha kirutubisho cha Fosforasi na ina jumla ya virutubisho 7 kulinganisha na mbolea zingine za kupandia, haichachushi wala udongo,huchochea uotaji wa mizizi mingi hivyo kuufanya mmea kuwa imara muda wote,huchochea machipukizi mengi  yanayoleta mavuno mengi  katika zao la mpunga.

Aidha amesema faida zingine ni kuyeyuka kwa haraka zaidi kwenye udogo na kufanya mmea upate vizurubisho vyake stahiki kwa muda unaohitajika
Pamoja  asilimia 50% ya ongezeko la uzalishaji kwa wakulima waliotumia.
 Meneja Masoko wa Kampuni ya Uzalishaji Mbolea ya  Yara , Linda Byaba akizungumza na waandishi habari kuhusiana na punguzo bei ya mbolea ya YaraMila Otesha leo jijini Dar es Salaam.
Meneja Masoko wa Kampuni ya uzalishaji Mbolea ya Yara , Linda Byaba akionyesha ubora wa mbolea aina ya YaraMila Otesha leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. namba kujua wapi nitapat mbolea za yara mimi ni mkulima mdgo nahitaji mbolea kwa matumizi ya bustani ndog ya nymbani.
    asante.
    emma.

    ReplyDelete
  2. Blogger unachekesha punguzo lipo wapi sasa? Mnaitia aibu tasnia ya uandishi wa habari

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...