Na Karama Kenyunko,Globu ya jamii
CHUO cha  Maliasili na Utalii jijini Dar es Salaam leo  kimewakabidhi vyeti Mama Lishe na madereva taksi 50 baada ya kuhitimu mafunzo ya utalii ikiwa ni muendelezo wa kukuza na kuboresha huduma za utalii nchini.

Akizungumza na wahitimu wa mafunzo hayo yaliyochukua takribani wiki moja katika ukumbi wa chuo hicho Dar es Salaam,  Mkurugenzi wa Jiji  Sporah Liana amesema, mafunzi hayo yatakuwa ni muendelezo wa kukuza shughuli za utalii nchini na kuongeza uelewa wa Mama lishe na madereva taksi ambao mara nyingi wamekuwa wakitoa huduma kwa watalii bila elimu ya kutosha

"Tumegundua shughuli za utalii zinafanyika katika kila kona ya Jiji hili, tumegundua pia watallii wanapenda kula chakula kwa Mama lishe kwani ambao wengi wao hawana mafunzo ya kutosha.

"Tunajua wanaofanya kwenye mahoteli makubwa wengi wao wanasoma katika Chuo hiki tofauti na mama lishe ambao hawana mafunzo yoyote, tumeonelea no vizuri na mama lishe pia tuwalete katika mafunzo  ili waweza kujua namna  ya kutoa huduma kwa watalii wetu" amesema Liana.

 Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Sporah Liana akizungumza alipokuwa anafunga mafunzo kwa wajasiriamali ambao ni mama lishe na madereva 50 baada ya kuhitimu mafunzo ya utalii ikiwa ni katika uboreshaji na kukuza huduma za utalii nchini.
Baadhi wahitimu wa mafunzo hayo ya utalii kwa wajasiriamali mama lishe na madereva wa taksi wakisikiliza nasaha za mgeni rasmi 

 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utalii Dr Shogo Mlozi Sedoyeka akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mafunzo hayo ambayo yatawasaidia wajasiriamali hao katika kutoa huduma zenye viwango na kuongeza thamani ya huduma zao.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...