Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
KAMPUNI ya Global Education Link imeamua kutoa ushauri nasaha wa kitaaluma kwa wanafunzi wa shule za sekondari mbalimbali nchini ili kuhakikisha wanafunzi wanafanikiwa kutimiza ndoto zao.

Imefafanua imeamua kutoa ushauri huo baada ya kuona wanafunzi wengi nchini hawana taarifa rasmi kuhusu vyuo vikuu na imesababisha wengi wao kushindwa kuchagua nini asome ili afanikishe malengo yake na matokeo kusababisha soko la ajira kuwa gumu.

Pamoja na hayo kampuni hiyo imesema ipo haja kwa Serikali kuunga mkono juhudi ambazo wamezianzisha katika kuhakikisha wanafunzi tangu wanapokuwa shuleni za msingi na sekondari wanajua mahitaji ya Taifa na nini asome ili kuwa na uhakika wa ajira.

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Global Education Link Abdulmalik Mollel wakati anazungumza na waandishi wa habari kuhusu uamuzi wa kampuni hiyo kutoa ushauri nahasa wa kitaaluma ambao wameanza na tano na kidato cha sita kwa shule za sekondari za Mkoa wa Dar es Salaam.

Amesema malengo yao ni kutoa ushauri huo kwa wanafunzi wote nchini kuanzia elimu ya msingi kwani ndiko ambapo watalaam wa Taifa hili wanaoanzia kuandaliwa.
 Mkurugenzi wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel akizungumza na wanafunzi walio fika kwenye semina hiyo.
 Mwanafunzi wa Shule  Sekondari Pugu,Christopher lyengwa akiuliza swali katika semeni hiyo iliyo fanyika katika ukumbu wa (GEL).
 Mkurugenzi Mkuu wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
Afisa  Elimu wa Mkoa wa Dar es salaam,Hamis Yusufu  Lissu akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi wa semina za kiwajegea uwezo  wanafunzi  wa Shule za Sekondari iliyoandaliwa na  Global Education Link (GEL).

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...