Na Mwandishi wetu
Washiriki wa mafunzo ya ufundi mitambo ya kurushia matangazo ya redio ambayo yameshirikisha mafundi kutoka redio jamii 25 zilizopo Tanzania Bara na Zanzibar wametakiwa kutumia vyema mafunzo ili yakalete mabadiliko katika maeneo yao ya kazi.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ufundi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Mwandisi Upendo Mbele wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo ya siku saba ambayo yameandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Mbele alisema mafunzo hayo ni muhimu kwa kuwa yatawapa uwezo wa kujua vifaa ambavyo wanavitumia katika vituo vyao na hivyo ni vyema wakayatumia vizuri ili yalete mabadiliko katika maeneo ya kazi.

"Ukiwa fundi mafunzo ni lazima, tuwashukuru UNESCO kuandaa mafunzo haya na nyie mtumieni muda wenu vizuri mkiwa hapa. Lengo kuu la kuwa hapa ni kujenga na kuboresha kile kitu ambacho hakikuwepo, unavyokuwa na upana zaidi na wewe utakuja kuwa mwalimu kwa wengine," alisema Mbele na kuongeza.
 Mkurugenzi wa Idara ya Ufundi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Mwandisi Upendo Mbele wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya ufundi mitambo ya kurushia matangazo ya redio kwa mafundi mitambo wa redio jamii 25 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ambayo yameandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).
 Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya ufundi mitambo ya kurushia matangazo ya redio kwa mafundi mitambo wa redio jamii 25 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ambayo yameandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).
 Washiriki wa mafunzo ya ufundi wa kurushia matangazo ya redio kwa mafundi mitambo wa redio jamii 25 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wakipewa maelezo kuhusu matumizi ya mitambo hiyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...