Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelezo ya ujenzi wa kituo maalumu ya Jeshi la Polisi cha Utalii na Diplomasia  jijini Arusha ambacho kimejengwa na wadau wa utalii  kwenye sherehe zilizofanyika leo Aprili 7, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na wadau waliosaidia  ujenzi wa kituo maalumu cha Jeshi la Polisi cha Utalii na Diplomasia  jijini Arusha  kwenye sherehe zilizofanyika leo Aprili 7, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe akiwa na viongozi wengine pamoja na wadau waliosaidia  ujenzi wa kituo maalumu cha Jeshi la Polisi cha Utalii na Diplomasia  jijini Arusha  kwenye sherehe zilizofanyika leo Aprili 7, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo  na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro  wakifunua pazia kuashiria kufunguliwa rasmi kwa nyumba za makazi ya askari ya polisi za Naura zilizojengwa upya baada ya kuteketea kwa moto kwenye sherehe zilizofanyika jijini Arusha leo Aprili 7, 2018.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaidiwa  na viongozi wengine akikata utepe  kuashiria kufunguliwa rasmi kwa nyumba za makazi ya askari ya polisi za Naura zilizojengwa upya baada ya kuteketea kwa moto kwenye sherehe zilizofanyika jijini Arusha leo Aprili 7, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na baadhi ya familia za askari polisi baada ya kufungua  rasmi nyumba za makazi ya askari ya polisi za Naura zilizojengwa upya baada ya kuteketea kwa moto kwenye sherehe zilizofanyika jijini Arusha leo


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride la askari polisi  katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha  kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya miaka 46 ya kifo cha Rais wa kwanza wa Zanzibar  Hayati Sheikh Abeid Amani Karume leo Aprili 7, 2018
Gari maalumu la kunyunyizia maji ya kuwashawasha likionesha namna kikosi cha kutuliza ghasia cha Jeshi la Polisi kinavyoweza kupambana na waandamanaji  katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya  siku ya kumbukumbu ya miaka 46 ya kifo cha Rais wa kwanza wa Zanzibar  Hayati Sheikh Abeid Amani Karume leo Aprili 7, 2018.   Aprili 7, 2018. 
 Askari wa Jeshi la Polisi wa kikosi maalumu cha kulinda viongozi wakionesha namna  kinavyoweza kupambana na maadui katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya  siku ya kumbukumbu ya miaka 46 ya kifo cha Rais wa kwanza wa Zanzibar  Hayati Sheikh Abeid Amani Karume leo Aprili 7, 2018 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...