WAZIRI
wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
amewataka waganga wakuu wote wa mikoa na wilaya nchi nzima kutenga siku
moja kwa mwezi kwa ajili ya uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi na
matiti kwa wanawake na tezi dume.
Waziri huyo ametoa agizo hilo mkoani Tanga leo wakati akizindua kampeni ya chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi na uchunguzi wa saratani kwa wakina mama katika kituo cha Afya cha Ngamiani jijini hapa.
Amesema kuwa hali ya saratani kwa nchi zinazoendelea haswa zilizopo kusini mwa jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania wagonjwa wa saratani wamekuwa wakiongezeka kila mwaka. Amesema kuwa Tanzania kunakuwa na wagonjwa 50,000 waliogunduliwa na tatizo la saratani.
Amesema kuwa katika wagonjwa hao asilimia 33 wanakutwa na saratani ya shingo ya kizazi na asilimia 12 wanagundulika na saratani ya matiti. Amebainisha kuwa kila katika wagonjwa 100,wagonjwa 80 wanakuwa katika hatua za mwisho za ugonjwa na kufanya matibabu kuwa magumu.
WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akizungumza leo Jijini Tanga wakati alipozindua kampeni ya chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi na uchunguzi wa saratani kwa wakina mama katika kituo cha Afya cha Ngamiani jijini hapa.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga ambaye ni Mkuu wa wilaya ya
Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni
hiyo
WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimuakifurahia jambo mara baada ya kuzindua kampeni hiyo ya chanjo
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga ambaye ni Mkuu wa wilaya ya
Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni
hiyo
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...