JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO


TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UFAFANUZI WA TAKWIMU ZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI NCHINI

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inapenda kutoa ufafanuzi wa takwimu za vifo vitokanavyo na uzazi nchini. Ufafanuzi huu unatokana na taarifa iliyorushwa na kituo cha Televisioni cha ITV katika moja ya taarifa zake za habari siku ya tarehe 29 Machi 2018 na baadaye kuanza kuzunguka katika mitandao ya kijamii inayosema “Shirika la Kimataifa la Idadi ya Watu-UNFPA limesema idadi ya vifo vya mama na mtoto vinavyotokana na uzazi hapa nchini imeongezeka hadi kufikia vifo 556 kwa kila vizazi hai elfu moja (1000) kutokana na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya afya ikiwamo uhaba wa wauguzi na wakunga”.

Nikiwa Waziri mwenye dhamana ya Afya, napenda kuufahamisha umma kuwa taarifa hizo sio sahihi.  Na ukweli wake ni kuwa takwimu za tathimini iliyofanywa na Taasisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) mwaka 2015/2016 (Ikiwa ni miaka miwili na nusu iliyopita) ya Hali ya Afya za Watu Tanzania (TDHS - MIS) ni kuwa vifo vya akinamama vitokanavyo na uzazi ni 556 kwa kila vizazi hai 100,000 (laki moja) na si vifo 556 kwa kila vizazi hai 1,000 (efu moja). Aidha nasisitiza kuwa Takwimu hizi ni za miaka miwili na nusu iliyopita.

Ni muhimu ikafahamika kuwa Serikali ya awamu ya Tano tangu imeingia madarakani Novemba 2015, imewekeza sana katika sekta ya afya hususani katika eneo la afya ya mama na mtoto. Tuna imani kuwa endapo itafanywa Tathmini kama hii iliyofanywa na kusimamiwa na Taasisi ya Taifa ya Takwimu  (NBS) hakuna shaka kuwa itatuonesha hatua kubwa tuliyopiga katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.
Serikali kwa kushirikiana na wadau wetu wa maendeleo tumechukuwa hatua mbalimbali zenye lengo la kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi. Mikakati ambayo serikali ya Awamu ya Tano kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya Afya imewekeza na kuitekeleza  ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi ni pamoja na:-

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...