Ajali ya hii imetokea majira ya saa mbili usiku wa jana huko kijiji cha Makomero wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora ambapo Basi lenye namba za usajili T.983 DCE mali ya Kampuni ya CITY BOY likiendeshwa na EMANUEL ATUPENDA CHITEMO mkazi likiwa linatokea Ngara Mkoa wa Kagera kuelekea Mkoa wa Dar es salaam liligongana na gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T.486 ARB lilokuwa linaendeshwa na SALUMU ABDALAH KALAMBO na kusababisha vifo vya abiria 12 huku 46 wakijeruhiwa.

Akiongea na waandishi wa Habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Kamishna Msaidizi Mwandamizi WILBROD MUTAFUNGWA ameeleza kwamba Abiria 12 walipoteza Maisha huku wengine 46 wakijeruhiwa na kati yao aliwataja abiria watatu ambao hali zao ni mbaya na wawili wamepelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando Mkoa wa Mwanza na mmoja Nkinga Mission wilaya ya Igunga.

Kamanda Mtafungwa ameeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni Gari aina ya Fuso kupasuka tairi ya mbele upande wa kulia na kusababissha kukatika kwa mfumo wa usukani likiwa katika mwendo mkali baada ya kuyaingia mashimo mawili yaliyo katikati ya barabara na kusababisha kupoteza mwelekeo na kisha kuligonga basi la abiria lililokuwa likipishana nalo.
Gari kampuni ya CITY BOY mara baada ya kupata ajali.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora alipowatembelea na kuwajulia hali majeruhi katika Hospitali ya Igunga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...