Timu 28 zinatarajia kushiriki Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) msimu wa 2017/18 inayotarajia kuanza Mei 1,2018 mpaka Mei 16,2018 kwenye vituo vinne. Vituo vitakavyotumika ni Geita, Singida, Rukwa na Kilimanjaro. 

Makundi ya RCL yatakuwa na timu saba kila kundi yakipangwa kwa kufuata Jiografia ya kikanda katika soka. 

Mwisho wa kuwasilisha jina la Bingwa wa Mkoa ilikua Machi 30, 2018 ambapo mikoa yote 26 iliweza kutimiza ndani ya muda huo uliowekwa na TFF.

Mikoa iliyothibitisha mabingwa wao wa RCL watakaocheza ligi hiyo msimu huu :

1. Dar Es salaam (Karume Market, Ungindoni FC, Temeke Squard)

2. Pwani (Stand FC)

3. Morogoro (Moro Kids)

4. Dodoma (Gwassa Sports Club)

5. Singida (Stand Dortmund)

6. Tabora (Tabora Football Club)

7. Kigoma (Red Stars FC)

8. Geita ( Gipco FC)

9. Kagera (Kamunyange FC)

10. Mwanza (Fathom Sports Club)

11. Mara (Nyamongo Sports Club)

12. Shinyanga (Zimamoto FC)

13. Simiyu (Ambassador FC)

14. Arusha (Bishoo Durning Sports)

15. Manyara (Usalama Sports Club)

16. Kilimanjaro (Uzunguni FC)

17. Tanga (Sahare All Stars)

18. Lindi (Majimaji Rangers)

19. Mtwara (Mwena FC)

20. Ruvuma (Black Belt)

21. Njombe (Kipagalo FC)

22. Songwe (Migombani FC)

23. Mbeya (Tukuyu Stars)

24. Iringa (Iringa United)

25. Rukwa (Laela FC

26. Katavi (Watu FC)

27.Manyara ()Usalama FC)

Mikoa ya Rukwa, Ruvuma na Tabora  kuna malalamiko ya vilabu kupinga mabingwa wa mikoa, malalamiko ambayo TFF inaendelea kuyafanyia kazi.

Kundi A (GEITA)

Geita, Kagera, Mara, Mwanza,Shinyanga, Simiyu, Dar 2

Kundi B (RUKWA)

Rukwa,Katavi, Kigoma, Tabora, Ruvuma, Songwe, Mbeya 

Kundi C (SINGIDA)

Singida,Dodoma,Iringa, Njombe, Dar 3, Lindi, Mtwara 

Kundi D (KILIMANJARO)

Kilimanjaro, Tanga, Arusha, Manyara, Pwani, Morogoro, Dar 1

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA TFF

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...