*Balozi wa Wang Ke aongoza Jumuiya ya marafiki wa China ,Tanzania kuwakumbuka waliopoteza maisha wakati wa ujenzi wa reli ya Tazara


Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

 SERIKALI ya Tanzania imeungana na Jamhuri ya Watu wa China katika kumbukumbu ya vifo vya Wachina 70 waliofarika wakati wa ujenzi wa reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA).

Watanzania waliongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Kikanda na Afrika Mashariki, Balozi Dk. Augustino Mahiga huku ikiwakilishwa na Balozi wao nchini, Wang Ke. Kumbukumbu hiyo, imeandaliwa na Jumuia ya Marafiki wa Tanzania na China ambayo Mwenyekiti wake Dk.Salim Salim na Katibu wake ni Joseph Kahama.

Kabla ya kuweka mashada kwenye makaburi kwenye makaburi ya wachina hao ambao wengi wao ni wataalamu na wahandisi katika ujenzi wa reli, ilitolewa historia fupi ya vifo vyao.

Akizungumza baada ya kuweka mashada, Balozi Mahiga alisema ujenzi wa reli hiyo ulithibitisha urafiki wa kutoka moyoni kati ya nchi hizo mbili na kufafanua ujenzi wake ulifungua milango kwa China kujenga viwanda vingine kama UFI na Kiwanda cha Nguo cha Urafiki."Wakati wa ujenzi huu damu zilimwagika, wachina wamepoteza maisha na wengine wamebaki na ulemavu wa kudumu...hivyo urafiki wetu sisi na China ni wa damu," amesema.

Naye, Balozi Wang amesema nusu ya karne iliyopita, kupitia ombi la Rais wa Tanzania, Julius Nyerere na Rais wa Zambia, Kenneth Kaunda, viongozi wa kizazi cha China, Mwenyekiti Mao Zedong na Waziri Mkuu, Zhou Enlai walifanya maamuzi ya kimkakati na kihistoria kusaidia ujenzi wa TAZARA.
 Mnara wa Makaburi ya Wachina waliokuwa wakijenga Reli ya Tazara  ambao walifariki wakati wa ujenzi wa reli hiyo miaka zaidi ya 40 iliyopita.
 Waziri wa Mambo ya Nje Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi  Agustine Mahiga akitoa heshima  na Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke, kwenye Mnara wa makaburi ya Wachina waliofkuja kutengeneza Reli ya Tazara
 Waziri wa Mambo ya Nje Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi  Agustine Mahiga akiwa na Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke, wakiongoza kuweka mashada ya maua kwenye moja ya kaburi la wakandarasi waliofika nchini kujenga reli ya Tazara
 Waziri wa Mambo ya Nje Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi  Agustine Mahiga  akihutubia Viongozi na wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliofika katika sherehe ya kitamaduni ya watu wa china ya kuwakumbuka mafundi waliojenga reli ya Tazara.
  Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke, akihutubia na kutoa historia fupi ya ushirikiano wa Tanzania na China ulivyoasisiwa na Mwalimu Nyerere.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...