Na Joel Maduka,Geita

Serikali imewahakikishia mazingira yaliyo salama wakulima wa zao la pamba ikiwa ni pamoja na kununuliwa kwa zao hilo bila ya kukopwa kwa msimu wa pamba ambao unatarajia kuanza tarehe 1 Mei mwaka huu .

Hayo yameelezwa na kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru , Charles Kabeho wakati akifungua mradi wa zao la pamba katika kijiji cha Nyamalimbe Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo alisema serikali imejipanga kuhakikisha mkulima wa pamba mwaka huu ananufaika na zao hilo.

“ Zao la Pamba linamanufaa kwa mkulima na serikali kwani zao ambalo linatengeneza nguo kuliko kusubili kuletewa mitumba kutoka nje hivyo tulithamini zao hili kwani linasaidia pia kuondoa umaskini katika familia”Alisisitiza Kabeho.

Mussa Kabehe ambaye ni Mkulima wa zao hilo alisema kwa sasa kutokana na hali ya hewa na mvua kunyesha kwa wingi wamekuwa na matumaini machache ya kupata pamba Nyingi kwani asilimia kuwa zimeharibikia shambani na kwamba awana matarajio ya kuzalisha pamba Nyingi zaidi ingawa kwa mwaka huu wengi walijitokeza kulima pamba.

Kiongozi huyo wa mwenge pia amefungua miradi 12 katika Halmashauli ya Wilaya ya Geita iliyo gharimu kiasi cha shilingi bilioni tano na milioni miatatu ambapo pia kiongozi huyo aliwakumbusha wananchi wa kijiji hicho kutojihusisha na suara la rushwa kwa ni adui wa haki.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Charles Kabeho akizungumza na kuwasisitiza wakulima wa zao la Pamba kuwekaza nguvu zaidi kulima zao hilo wakati alipoweka Jiwe la Msingi kwenye mradi wa shamba la pamba kijiji cha Nyamalimbe Wilayani Geita. 
Baadhi ya pamba zikiwa shambani kabla ya kuvunwa. 
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Charles Kabeho,akiweka jiwe la msingi kwenye shamba la pamba kwenye kijiji cha Nyamalimbe. 
Watoto ambao ni yatima wakipewa zawadi na Kiongozi wa mbio za mwenge Charles Kabeho kwenye Kijiji cha Bujura wilayani Geita. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...