Na Mwamvua Mwinyi,Bagamoyo
Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani inafanya tathmini ya mafuriko ya mvua yaliyotokea ili waweze kununua dawa kwa ajili ya kuua wadudu wanaoweza kuleta magonjwa mbalimbali yatokanayo na kutuama kwa maji ya mvua.
Hayo yalisemwa Bagamoyo na mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Fatuma Latu wakati wa kikao cha baraza la madiwani.Latu alisema kutokana na tatizo la maji kutuama katika maeneo mengi yakiwemo kwenye makazi ya watu,inabidi kuwekwa dawa ya kuua wadudu hao .
Aidha alieleza athari za mvua ni kubwa , kila kata kupitia madiwani wamekubaliana na madiwani ,kamati husika zitakaa ili kufuatilia suala hilo.Latu alisema kuwa suala hilo lililetwa kwenye baraza kama dharura kutokana na hali ya mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini.
Awali Diwani wa kata ya Makurunge Paul Kabile alisema kuwa mvua hizo zimeleta athari kubwa sana kwa wananchi ambapo wamezungukwa na maji ambayo yanaweza kuleta athari ya magonjwa ya mlipuko.Kabile alisema ,athari ni kubwa ambapo baadhi ni uharibifu wa makazi,barabara,miundombinu mbalimbali hali inayofanya wananchi wawe na wakati mgumu kuingia au kutokana kwenye majumba yao.
Naye Diwani wa viti maalum Shumina Abdala alisema kuwa licha ya makazi kuathiriwa na mvua hizo hata taasisi za umma kama shule,zahanati na vituo vya afya.Abdala alisema kuwa kuna haja ya kuwa na dharura juu ya suala la kupatikana dawa za kuwa wadudu wanaoweza kuleta magonjwa kwani uchafu umetapakaa kila mahali.
Mkurugenzi halmashauri ya Bagamoyo,Mkoani Pwani Fatuma Latu akizungumza katika baraza la madiwani.
Baadhi ya madiwani wa wilaya ya Bagamoyo, wakifuatilia kwa makini yaliyojiri katika baraza la madiwani wilayani hapo
Diwani wa viti maalum ,Shumina Abdala (mwenye aliyeaimama mwenye blauzi yekundu)akizungumza jambo wakati wa baraza la madiwani wilayani Bagamoyo.Picha na Mwamvua Mwinyi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...