Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Taasisi ya Mkakati wa Uwajibikaji na Uwazi katika Sekta Ujenzi (COST) imesema kuwa itaendelea kushirikiana na taasisi nunuzi katika sekta ya ujenzi kuangalia uwajibikaji na uwazi katika ujenzi wa miradi mbalimbali.
Hayo ameyasema Mwenyekiti wa Taasisi ya COST, Mhandisi Kazungu Magili wakati wa mkutano wa Sita wa Mwaka wa Taasisi hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam, amesema kuwa kazi ya COST kuangalia miradi ya ujenzi kuwa na uwajibikaji na uwazi ili wananchi kuweza kupata ujenzi bora wa miundombimu mbalimbali inayojengwa nchini.
Amesema kuwa uwajibikaji na uwazi wa nguzo katika kupima thamani ya fedha inayoendana na miundombinu mbalimbali inayotekelezwa nchini.
Magili amesema wadau wana kazi ya kufatilia taarifa katika miradi katika kuweza kufatilia ujenzi wa miundombinu na ndipo umma utatambua uwajibikaji katika rasilimali zao.
Amesema kuwa COST itaendelea kungalia miradi ya miundombinu kuhakikisha taarifa zake zinapatikana kwa kila mdau kwa kila hatua za ujenzi wa mindombinu hiyo.
Sekta ambazo za ununuzi zinazoshirikiana na Tanroad , Tarura pamoja na taasisi ambazo zinasheria katika kufatilia manunuzi ili kuweza kufanya uwajibikaji na uwazi.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mkakati wa Uwajibikaji na Uwazi katika Sekta Ujenzi (COST),Mhandisi Kazungu Magili akizungumza katika mkutano wa sita wa taasisi hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.
.Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya COST, Alhaj Arch Jehad Jehad akizungumza na wajumbe wa COST katika mkutano wa sita wa mwaka uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja wajumbe na viongozi wa COST katika mkutano wa sita wa mwaka uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...