Na Veronica Simba – Dodoma
Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani na Naibu Waziri Subira Mgalu wameongoza kikao kilichojadili maendeleo ya Mradi wa Gesi ya Kusindikwa (LNG).
Kikao hicho kilifanyika Aprili 30 mwaka huu Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma na kushirikisha Mabalozi wa nchi za Norway, Uingereza na Uholanzi pamoja na Kampuni mbalimbali za utafutaji wa mafuta kwa ajili ya Mradi wa LNG, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (EWURA), Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) na wataalamu kutoka wizarani.
 Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani (kushoto) akiongoza kikao kujadili maendeleo ya Mradi wa Gesi ya Kusindikwa (LNG), kilichofanyika Aprili 30 mwaka huu, Makao Makuu ya Wizara Dodoma. Kulia ni Naibu Waziri Subira Mgalu.
 Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani na Naibu Waziri Subira Mgalu (kushoto), wakiongoza kikao kujadili maendeleo ya Mradi wa Gesi ya Kusindikwa (LNG), kilichofanyika Aprili 30 mwaka huu, Makao Makuu ya Wizara Dodoma. Wengine pichani ni Mabalozi wa nchi za Norway, Uingereza na Uholanzi, wawakilishi wa Kampuni mbalimbali za utafutaji wa mafuta kwa ajili ya Mradi wa LNG, wajumbe kutoka TPD, EWURA na PURA.

 
 Mabalozi wa nchi za Norway, Uingereza na Uholanzi pamoja na  wawakilishi wa Kampuni mbalimbali za utafutaji wa mafuta kwa ajili ya Mradi wa LNG, wakiwa katika kikao hicho.
Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani akisalimiana na Mabalozi wa nchi za Norway, Uingereza na Uholanzi pamoja na  wawakilishi wa Kampuni mbalimbali za utafutaji wa mafuta kwa ajili ya Mradi wa LNG, muda mfupi kabla ya kuanza kikao baina yao kujadili maendeleo ya Mradi huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...