Kamati ya bunge ya hesabu za Serikali za Mitaa kutoka Nchini Uganda (PAC-LG) imemwagia sifa Mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es salaam unaoendelea kutekelezwa katika Manispaa ya Tano za Mkoa wa Dar es salaam. 

Kamati hiyo yenye zaidi ya wajumbe kumi waliotemebelea Mradi wa DMDP unaotekelezwa chini ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa wamesema ni mradi wa mfano na kuigwa na Nchi za Afrika Masshariki zinazopata mkopo wa fedha kutoka Benki ya Dunia.

Akizungumza katika ziara hiyo ya mafunzo Mwenyekiti wa Kamati hiyo (PAC-LG) Mhe. Ronald Reagan Okumu amesema lengo la ziara yao ni kuona namna ambavyo miradi ya Uboreshaji Miundombinu inayotekelezwa kwa fedha za Mkopo toka Benki ya Dunia;

“Tunapenda kuona ubora wa miradi hiyo, taratibu za ulipaji fidia zilivyofuata, maelekezo ya mkopo wa fedha hizo yalivyozingatiwa na zaidi namna ambavyo fedha zilivyopokelewa, zinavyosimamiwa na wataalamu, zinavyotumika na zinafanyiwa ukaguzi na zaidi suala zima la thamani ya fedha”Value for Money” kuonekana katika miradi hiyo” alisema Mhe. Okumu.
Naibu Waziri OR-TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege (kushoto) akiwapokea wajumbe wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa toka Nchini Uganda waliotembela Wizara kuona ubora wa miradi ya Benki ya Dunia inavyotekelezwa. 
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa toka Uganda (PAC-LG) Mhe. Ronald Reagan Okumu (kulia) akiwa na mjumbe wa Kamati hiyo toka Uganda wakifuatilia kikao na Naibu Waziri wa Tamisemi(hayupo pichani) Mhe. Joasephat Kandege. 
Naibu Waziri OR-TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege akifurahia jambo wakati wa kikao cha Mapokezi ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa. 
Wataalam wanaosimia Miradi ya Benki ya Dunia OR-TAMISEMI pamoja na Kamati ya Bunge ya hesabu za Serikali za Mitaa toka Uganda wakimskiliza mtaalamu wa maabara ya mradi wa DMDP 
Wataalam wanaosimia Miradi ya Benki ya Dunia OR-TAMISEMI pamoja na Kamati ya Bunge ya hesabu za Serikali za Mitaa toka Uganda wakimskiliza mtaalamu wa maabara ya mradi wa DMDP 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...