Malezi bora katika familia imesemeka ni ndio msingi wa malezi kwa watoto katika jamii yetu hivyo wazazi wanapaswa kuzingatia kutoa malezi bora kwa watoto ndani ya familia na jamii kwa ujumla ili kuwa na taifa lenye uchu wa kujiletea maendeleo.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe.Vaileth Makota wakati akisoma Hotuba ya Wziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika maadhimisho ya Siku ya Familia Duniani yaliyofanyika Wilayani Kondoa katika Mkoa wa Dodoma.
Mhe. Vaileth Makota amesema kuwa wazazi wanawajibu wa kuwalea watoto katika malezi bora na katika maadili mazuri ili kujenga taifa bora lenye watoto wanaojitambua, wanaojithamini, na wenye maadili mema ili kulitumikia Taifa.
Ameongeza kuwa wazazi wanatakiwa kuwa walimu kwa matendo yao kwa watoto kwani watoto wanaiga yale ambayo wazazi wanafanya hivyo tabia na mienendo yao ni kati ya vitu ambavyo vitasababisha malezi mabaya au bora kwa watoto na jamii kwa ujumla.
Mkuu
wa Wilaya ya Kondoa Mhe.Vaileth Makota akiwasisitiza wazazi kuchangia
ujenzi wa famila na taifa kwa kuwapa malezi bora watoto wakati wa
maadhimisho ya Siku ya Familia Duniani iliyofanyika Wilayani Kondoa
katika Mkoa wa Dodoma.
Mkurugenzi
wa Maendeleo ya Mtoto Bibi Magreth Mussai akizungumzia umuhimu wa
malezi bora katika familia na wajibu wa wazazi katika kutoa malezi hayo
wakati wa maadhimisho ya Siku ya Familia Duniani iliyofanyika Wilayani
Kondoa katika Mkoa wa Dodoma.
Mkuu
wa Wilaya ya Kondoa Mhe.Vaileth Makota( wa pili kushoto) akipokea bango
la wadau kutoka nchi za ulaya wanaounga mkono jitihada za Serikali ya
Tanzania kupinga ndoa za utotoni wakati wa maadhimisho ya Siku ya
Familia Duniani iliyofanyika Wilayani Kondoa katika Mkoa wa Dodoma.
Nesi
akimchoma mtoto wa Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Vanessa Makota Chanjo ya
Saratani ya Shingo ya Kizazi katika uzinduzi wa chanjo hiyo Wilayani
Kondoa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Familia Duniani iliyofanyika
Wilayani humo.
Wanafunzi
na Wananchi wa Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma wakifuatilia mambo
mbalimbali katika Siku ya Familia Duniani yaliyokuwa yakifanyika katika
Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...