Na Imani Hezron, Adventist
Mkutano wa Ufunuo wa Matumaini unaendelea katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza ambapo mafundisho ya Afya, Kaya, Familia na neno la Mungu yanafundishwa. Muhubiri Mkuu kwenye mkutano huo ulioanza Mei 12, 2018 ni Mchungaji Dkt.Mark Finley kutoka Marekani.
Mkutano huo unaanza kila siku kuanzia saa 16:00 alasiri hadi saa 20:00 usiku huku pia yakikujia mubashara kupitia Hope Chanel Tanzania kwenye visimbuzi vya Continental pamoja na Ting bila kusahau kwenye Youtube. Pia yanapatikana 102.1 Morning Star Radio Mwanza na kwenye programu tumishi (Application) za Itune na TAMC.
Kupitia BMG, Karibu kusikiliza wimbo maalumu wa mkutano huo kutoka kwa vijana wa Melodies of Hope.
Waimbaji wa Melodies of Hope wakiimba wimbo maalumu kwenye mkutano wa Ufunuo wa Matumaini Jijini Mwanza.
Mkutano huu ulifunguliwa rasmi Mei 13, 2018 na Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe.Dkt.Mwigulu Nchemba.
Sikiliza wimbo maalum wa mkutano huu hapa chini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...