Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika fainali ya kutafuta watangazaji watatu wenye vipaji kati ya 30 itakayofanyika Mei 12 mwaka huu katika ukumbi Dar Live jijini Dar es Salaam.
Akizuungumza leo Dar es Salaam, Ofisa Uhusiano wa Times FM Radio, Flora Matthew amesema walioshiriki katika shindano la kusaka vipaji walikuwa watu 1000 na baadae wamechujwa na kufikia 30 ambao wanaingia katika fainali ya kutafuta washindi watatu.
Amesema kuwa washindi hao watasomeshwa na radio hiyo kwa lengo la pata taaluma ya habari kutokana na sheria ya utangazaji inavyotakiwa. Frola amesema washiriki 27 wataobakia ni wazuri lakini mahitaji ya shindano ya watangazaji wa wenye vipaji ilikuwa inahitaji watangazaji watatu.
Fainali zitaambatana na burdani mbalimbali kwa wasanii ambao ni Barnaba Classic , Khadija Kopa, Country Boy, QBoy, Chemical Whitnes na Ochu, Cheen Bees , Nchama , Enock Bella, Whozu , Kisamaki na Getu wengine Young Tuso, Jovi , Mabantu , Orbit na wengi ambao watakuwepo katika fainali hizo.
Amesema kiingilio cha fainali ya hizo ni sh. 5000 katika kuwashudia washindi watatu wataoibuka.
Ofisa Uhusiano wa Times FM Radio, Flora Matthew akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na fainali ya kusaka vipaji iliyokuwa inaendeshwa na radio hiyo leo jijini Dar es Salaam
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...