Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni amekabidhi vifaa vya michezo kwa Timu 20 zinazoshiriki ligi ya Masauni and Jazeera Cup.
Akizungumza wakati akikabidhi vifaa hivyo Masauni amesema michezo inajenga udugu kutokana na mkusanyiko wa watu mbalimbali.
Masauni amesema michezo kwa sasa ni ajira kwani wengine wataonyesha vipaji vyao na timu zikawaona na zikaweza kuingia nao mikataba.
Aidha amesema kwake ataona faida pale baadhi ya vijana watakaonyesha vipaji na timu zikawachukua.
Aidha amesema ataendelea kuwa bega kwa bega na vijana kwa kudhamini ligi mbalimbali zitaanzishwa katika jimbo la Kikwajuni
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani,Hamad Masauni akikabidhi vifa vya michezo jezi na Mpira kwa timu 20 zinazoshiriki ligi ya Masauni na Jazeera Cup katika Jimbo la Kiwajuni
 Sehemu ya vifaa vya michezo.
Baadhi ya viongozi wa tumu mbalimbali wakiwa wameshika jezi za timu zao zinazoshiriki ligi ya Masauni na Jazeera Cup katika Jimbo la Kiwajuni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...