Na Ripota Wetu, Globu ya jamii
BALOZI wa Tanzania nchini China Mbelwa  Kairuki kwa niaba ya Makao Makuu ya Jeshi amemvisha  rasmi Kanali R.C Ng’umbi  cheo kipya cha  Brigedia Jenerali.

Brigedia Jenerali Ng’umbi  ambaye pia ni Mwambata Jeshi katika Ubalozi wa Tanzania  nchini China , ni miongoni mwa maofisa  27 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliopandishwa vyeo  tarehe 12 Aprili mwaka ,2018 na Rais na Amiri Jeshi  Mkuu Dkt. John Magufuli.

 Akizungumza Mara baada ya kuvalishwa Cheo hicho jana Mei 7 , Brigedia Jenerali  alimshukuru Amiri Jeshi Mkuu  Dk. Magufuli  pamoja na uongozi wa Makao Makuu ya Jeshi kwa kupandishwa cheo kuwa Brigedia Jenerali.

Tukio hilo lilifanyika  katika ofisi za  ubalozi wa Tanzania nchini China  na kuhudhuriwa na maofisa  pamoja na watumishi  kutoka ofisi  za Ubalozi  pamoja na familia zao.
 Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa  Kairuki kwa niaba ya Makao Makuu ya Jeshi akimvisha  rasmi Kanali R.C Ng’umbi  cheo kipya cha  Brigedia Jenerali katika hafla iliyofanyika kwenye ubalozi wa Tanzania nchini China.
  Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa  Kairuki, Brigedia Jenerali, R.C Ngumbi  wakiwa katika picha ya pamoja  na Maafisa na Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China.
  Brigedia Jenerali R.C Ngumbi akiwa katika  picha ya pamoja  na Balozi Mbelwa Kairuki, Maafisa na Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...