Na  Bashir  Yakub.

Ume;muuzia mtu kiwanja au nyumba. Mmeandika mkataba na kuusaini tena mbele ya mwanasheria. Kwenye mkataba mmeweka vipengele vingi  lakini kimojawapo kinahusu umaliziaji wa pesa ya manunuzi.  Hii ni kwasababu mnunuzi amelipa kiasi kidogo na kiasi kingine ameahidi kwenye mkataba kukimalizia baada ya muda fulani.

Mkataba umesainiwa na umekamilika. 

Mda umeenda na kufika ule ambao mnunuzi alitakiwa kumalizia kiasi kilichobaki  lakini bado haoneshi dalili za kumalizia kiasi hicho.  Umejaribu kumkumbusha mara kadhaa lakini maneno yake ni yaleyale  na pesa halipi.  Muda mlioahidiana sasa umepita lakini bado  mnunuzi hajamalizia hela .  Na pengine sasa hapokei hata simu  au hujui aliko au anatoa majibu ya dharau au yasiyoridhisha au vinginevyo.
Nini ufanye katika mazingira kama haya, zipi haki zako, ipi hadhi ya mkataba wenu wa mauziano ambao uliusaini nk, nk. Tutaona hapa chini.

1.KUHUSU KUUZIANA NA KUBAKI NA DENI.
Sheria haikatazi kuuziana ardhi na likabaki deni. Suala hilo limeachwa katika hiari ya muuzaji na mnunuzi.Ni wao watakoamua kuhusu kulipa hela yote au kulipa kiasi na kubaki na deni.  Kifungu cha 10 cha Sheria ya Mikataba kimesema  mkataba ni halali ikiwa umefanywa na wahusika timamu/kamili,huku wakiuziana kitu halali, na kwa masharti  halali ya kisheria. Basi madhali haya yametimia  jambo la kubaki na deni halikatazwi kisheria.

KUSOMA ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...