Na
Bashir Yakub.
Ume;muuzia mtu kiwanja au nyumba. Mmeandika mkataba na
kuusaini tena mbele ya mwanasheria. Kwenye mkataba mmeweka vipengele vingi lakini kimojawapo kinahusu umaliziaji wa pesa
ya manunuzi. Hii ni kwasababu mnunuzi
amelipa kiasi kidogo na kiasi kingine ameahidi kwenye mkataba kukimalizia baada
ya muda fulani.
Mkataba umesainiwa na umekamilika.
Mda umeenda na kufika ule
ambao mnunuzi alitakiwa kumalizia kiasi kilichobaki lakini bado haoneshi dalili za kumalizia
kiasi hicho. Umejaribu kumkumbusha mara
kadhaa lakini maneno yake ni yaleyale na
pesa halipi. Muda mlioahidiana sasa
umepita lakini bado mnunuzi hajamalizia
hela . Na pengine sasa hapokei hata
simu au hujui aliko au anatoa majibu ya
dharau au yasiyoridhisha au vinginevyo.
Nini ufanye katika mazingira kama haya, zipi haki zako, ipi
hadhi ya mkataba wenu wa mauziano ambao uliusaini nk, nk. Tutaona hapa chini.
1.KUHUSU KUUZIANA NA
KUBAKI NA DENI.
Sheria haikatazi kuuziana ardhi na likabaki deni. Suala hilo
limeachwa katika hiari ya muuzaji na mnunuzi.Ni wao watakoamua kuhusu kulipa
hela yote au kulipa kiasi na kubaki na deni.
Kifungu cha 10 cha Sheria ya Mikataba kimesema mkataba ni halali ikiwa umefanywa na wahusika
timamu/kamili,huku wakiuziana kitu halali, na kwa masharti halali ya kisheria. Basi madhali haya
yametimia jambo la kubaki na deni
halikatazwi kisheria.
KUSOMA ZAIDI sheriayakub.blogspot.com
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...