Serikali imekutana na wadau wa Maendeleo Jijini Dar es Salaam kujadiliana kuhusu utekelezaji wa Sera na Mipango ya kitaifa inayohusu masuala ya jinsia ikiwemo Mpango wa Kitaifa wa Kutokomeza vitendo  vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto  (2017/18 – 2021/22); utekelezaji wa mikataba ya kikanda na kimataifa kuhusu kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa Wanawake kiuchumi. 

Akizungumza katika kikao kati ya Serikali na wadau hao Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Sihaba Nkinga amesema Serikali imeamua kukutana na wadau ili kujadiliana na kupata maoni kuhusu utekelezaji wa Sera Mipango na mikakati ya Serikali katika masuala ya kijinsia ili kuweza kutekeleza kwa mafanikio masuala hayo.

Ameongeza kuwa Serikali inashirikiana na wadau wa Maendeleo kwa karibu ili kuwa na Mipango na  mikakati ya pamoja ya kutekeleza masuala mbalimbali ya kijinsia ikiwemo kutokomeza vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto na uwezeshaji wa Wanawake kiuchumi.

"Ni jambo la busara kuwashirikisha wadau wa Maendeleo katika masuala ya kimaendeleo ili kupeleke mbele kurudumu la maendeleo" alisisitiza Bi. Sihaba.
 Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Sihaba Nkinga akizungumza na wadau wa Maendeleo Jijini Dar es Slaam wakati wa majadiliano kuhusu utekelezaji wa Sera na mipango ya kitaifa inayohusu masuala ya jinsia ikiwemo Mpango wa Kitaifa wa Kutokomeza Vitendo vya  Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (2017/18 – 2021/22); utekelezaji wa mikataba ya kimataifa kuhusu kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake kiuchumi. Kulia ni Mwakilishi wa UN Women nchini Bi. Susan Steffen.
 Mwakilishi wa UN Women nchini Bi Susan Steffen  akielezea Mipango ya Umoja wa Mataifa katika kuwezesha masuala ya Kijinsia na uwezeshaji wa wanawake  kiuchumi wakati wa kikao kati ya Serikali na wadau wa Maendeleo Jijini Dar es Slaam kujadiliana kuhusu utekelezaji wa Sera na mipango ya kitaifa inayohusu masuala ya jinsia ikiwemo Mpango wa Kitaifa wa Kutokomeza vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto  (2017/18 – 2021/22) ; utekelezaji wa mikataba ya kikanda na kimataifa kuhusu kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake kiuchumi. Kushoto ni Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga.
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango Bw. Atupele Mwambene akielezea kuhusu utekelezaji wa Mipango wa Kitaifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto  (2017/18 – 2021/22) (NPA) katika kikao kati ya Serikali na wadau kujadiliana kuhusu utekelezaji wa Sera na mipango ya kitaifa inayohusu masuala ya jinsia ikiwemo Mpango wa Kitaifa wa Kutokomeza vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto  (2017/18 – 2021/22) ; utekelezaji wa mikataba ya kikanda na kimataifa kuhusu kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa Wanawake kiuchumi.
 Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Idara ya Maendeleo ya Jinsia Bi.Dorah Neema akielezea kuhusu masuala ya  Kamisheni ya hali ya Wanawake (CWS) katika kikao kati ya Serikali na wadau kuhusu utekelezaji wa Sera na mipango ya kitaifa inayohusu masuala ya jinsia ikiwemo Mpango wa Kitaifa wa Kutokomeza vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto  (2017/18 – 2021/22) , utekelezaji wa mikataba ya kimataifa kuhusu kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa Wanawake kiuchumi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...