Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 
SERIKALI imetangaza nafasi za ajira katika sekta ya afya 6,180 katika kuhakikisha kuwa upungufu wa watumishi wa kada ya afya inatatuliwa na kuimarika katika upatikanaji wa huduma bora ya afya nchini.
Akitangaza ajira hizo leo jijini Dar es Salaam Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Tawala za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo amesema watakapoajiriwa watumishi hao watapangiwa katika maeneo mbalimbali ya nchi kwa kuzingatia uhitaji.
"Watumishi watakaoajiriwa katika sekta ya afya ni madaktari, wafamasia wauguzi , Tabibu pamoja na wahudumu wa afya.Wenye sifa za taaluma za afya wajitokeze kuomba nafasi hizo ili waweze kuajiriwa na kutoa huduma kwa wananchi,"amesema Jafo na kuongeza vigezo  vyote vya waombaji vitazingatiwa ili kutoa huduma bora za afya kutokana na taaluma walizosomea.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Tawala za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati anatangaza ajira hizo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...