Sherekea Sanaa ni tamasha la kipekee linalosheherekea sanaa na tamaduni za Tanzania kwa njia ya mziki, miondoko, michoro na mengineyo. Nafasi Art Space inawaalika tarehe 2 Juni kuanzia saa 12.30 joini mpaka saa 5 usiku kwenye tamasha hili linalofanyika kwa ushirkiano wa Nordic Week.

Siku hio, ndani ya ukumbi wa Nafasi Art Space, kutakuwa na maonyesho ya sanaa ya “Silence (ukimya)” zilizoandaliwa na wasanii mbali mbali nchini. Na kwenye jukwaa makundi ya “Muda Dance” na “Nantea Dance” yameandaa maonyesho yao ya miondoko ya kisasa, yaani contemporary dance.

Aidha, kwaya maarufu kutoka Denmark inaojulikana kama Nordlys Choir wataburudisha wahudhuria. Pia dada Grace Matata atakuwepo kuwafuharisha mashabiki wa miziki wa kizazi kipya.
Hivyo kutakuwa na kitu kwa kila mmoja. Tamasha hili la SHEREKEA SANAA ni bure na wote mnaalikwa.

Tuma Barua pepe info@nafasiartspace.org kujua zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...