Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii

Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Manchester United, Sir Alex Ferguson imebainika amefanyiwa Upasuaji katika Ubongo wake baada ya hapo awali kuripotiwa kuumwa ghafla.

Manchester United kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter imetoa taarifa ya kuumwa kwa Sir Ferguson kwa kusema kuwa "Tayari ameingia kufanyiwa upasuaji wa Ubongo wake na zoezi linaendelea vizuri lakini anahitaji kuwa katika Uangalizi maalum kwa msaada ili arudi katika hali yake ya kawaida".

Kabla yakuumwa, Sir Alex Ferguson hapo nyuma alinekana katika mchezo kati ya Man United dhidi ya Arsenal, Old Trafford wakati wakumuaga Kocha wa Washika Mitutu wa London (Gunners), Arsene Wenger anayeondoka klabuni hapo mwishoni mwa msimu huu.


Sir Alex Furguson alishinda Mataji 13 ya Ligi Kuu Soka nchini Uingereza katika kipindi cha miaka 26 alipokuwa akiifundisha Manchester United kabla yakustaafu mwaka 2013.

Chanzo: Goal. com
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...