Wajumbe wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA) wakifatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Mhadhiri wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Charles George Magaya katika siku ya kwanza ya Mkutano wao, unaofanyika kwenye Ukumbi wa Chuo Kikuu Zanzibar (SUZA), Tunguu, Zanzibar. ambapo alisema kuwa Kada ya Makatibu Mahsusi ni kati ya kada kongwe kabisa katika historia ya Utumishi Serikalini, Taasisi za umma hata kwenye Sekta binafsi. Ni dhahiri Watendaji Wakuu na Viongozi wengi sehemu ya kazi wamekuwa wanauhitaji utendaji mzuri wa Katibu Mahsusi ili wafanye kazi zao kwa haraka na ufanisi zaidi.
Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA), Zuhura Maganga akizungumza jambo katika siku ya kwanza ya Mkutano wao, unaofanyika kwenye Ukumbi wa Chuo Kikuu Zanzibar (SUZA), Tunguu, Zanzibar.
Sehemu ya Wajumbe wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA) wakifatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika siku ya kwanza ya Mkutano wao, unaofanyika kwenye Ukumbi wa Chuo Kikuu Zanzibar (SUZA), Tunguu, Zanzibar.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...