Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii
NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega amezindua msikiti kwa kisasa ujulikanao kama Maajid Habresh katika kijiji cha Tengelea huko Mkuranga.
Uzinduzi huu umefanyika leo ambapo ulienda sambamba na ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika jimbo lake na kusikiliza maoni na kujibu maswali kutoka kwa wananchi.
Ulega amesema ni jukumu lao kusimamia maendeleo ya wananchi hasa katika elimu na amehaidi kusaidia katika kujenga madarasa na hawatachoka kumuunga mkono jitihada za Rais Magufuli na wananchi kwa ujumla.Aidha ameeleza wananchi wa kijiji cha Kazole wajiandae kupata huduma ya umeme ikiwa na mkakati wa kuwapa huduma bora.
Katika ziara hiyo Ulega ametoa mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya Kazole, na ametoa kiasi cha shilingi laki tatu kwa kikundi cha wajasiriamali kwa wanawake cha Thirty family vicoba sambamba na kuwasalimu wananchi wa Mkuranga na kuwaomba wananchi wasizuie miradi ya maendeleo na kuitunza miradi hiyo.
Muonekano wa msikiti aliuzindua Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi,Abdullah uliopo katika kijiji cha Tengelea Wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani. (Picha zote na Emmanuel Massaka, Globu ya jamii)
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah ulega akikabidhi mifuko ya saruji mia moja kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Kazole.
Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi na mbunge wa Mkuranga,Abdallah Ulega akishiriki shughuli ya ujenzi wa madarasa ya shule ya msingi Kazole ambapo akimkabidhi mifuko mia moja ya Saruji.
Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi na mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akigawa tende kwa waumini wa Msikiti huo mara baada uliopo k katika kijiji cha Tengelea mkoa wa Pwani.
Naibu waziri wa mifugo na uvuvi na mbunge wa jimbo la mkuranga Abdallah Ulega akizungumza na waumini wa msikiti wa Habresh mara baada ya kuzindua msikiti huo uliopo katika kijiji cha Tengelea mkoa wa Pwani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...