Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari - MAELEZO, Rodney Thadeus akifafanua jambo mbele ya watumishi wa Idara hiyo walipokutana na ujumbe kutoka Shirika la Simu Tanzania (TTCL) kwa ajili ya kujengewa uelewa kuhusu huduma za Shirika hilo leo Jijini Dar es Salaam.Kutoka kulia ni Afisa Mauzo wa TTCL, Bi. Rahel Mremi na Esther Killango. TTCL ni shirika la Serikali linalotoa huduma za mawasiliano likiwa na kauli mbiu "Rudi Nyumbani Kumenoga."
 Afisa Mauzo wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL), Bi. Rahel Mremi akionyesha Line za TTCL mbele ya Watumishi wa Idara ya Habari -MAELEZO walipotembelea ofisi za Idara hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari - MAELEZO, Rodney Thadeus na Afisa Mauzo wa TTCL, Esther Killango(kushoto).
 Afisa Mauzo wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL), Bi. Esther Killango akifafanua jambo mbele ya Watumishi wa Idara ya Habari -MAELEZO walipotembelea ofisi za Idara hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Msaidizi wa Mauzo wa TTCL, Bi. Damiana Shemweta, Afisa Mauzo wa TTCL, Bi. Rahel Mremi na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari - MAELEZO, Rodney Thadeus(wapili kutoka kushoto). 
 Baadhi ya watumishi wa Idara ya Habari - MAELEZO, kituo cha Dar es Salaam wakifuatilia maelezo kuhusu huduma na bidhaa zinazotolewa na Shirika la Simu Tanzania (TTCL) walipotembelewa na maafisa mauzo kutoka shirika hilo leo Jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mauzo wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL), Bi. Rahel Mremi akionyesha moja ya aina ya simu zinazotumika kwa ajili ya huduma ya sauti mbele ya watumishi wa Idara ya Habari -MAELEZO walipotembelea ofisi za Idara hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari - MAELEZO, Rodney Thadeus(katikati) na Afisa Mauzo wa TTCL, Esther Killango.
Msaidizi wa mauzo toka Shirika la Simu Tanzania (TTCL), Bi. Damiana Shemweta akigawa vipeperushi vyenye maelezo ya huduma na bidhaa za shirika hilo kwa watumishi wa Idara ya Habari -MAELEZO leo Jijini Dar es Salaam. (Picha na: Frank Shija - MAELEZO)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...