Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amezindua mashindano ya shule za sekondari ya Copa Umisseta mjini Bukoba. 

 Akizindua mshindano hayo mwishoni mwa wiki iliyopita katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Dkt. Mwakyembe ambaye alikuwa mgeni rasmi amesema michezo ni burudani, inaleta undugu, umoja na upendo hivyo h aina budi kuienzi siku zote. "Nawaomba vijana mpende michezo maana ni burudani na ilateta afya kwa watu wa rika zote, mkizingatia hivyo hakutakuwa na watu wenye magonjwa ya ajabu ajabu," amesema. 

 Mashindano hayo yalipambwa na shamrashamra mbalimbali za michezo na burudani katika uwanja wa Kaitaba na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali, wadau wa michezo na wanzi wa shule za sekondari na mgeni rasmi alikuwa ni Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe, aliyeambatana na Mkuu wa Wilaya ya Muleba, Mhandisi Richard Ruyango, aliyemwakilisha Mkuu wa mkoa wa Kagera pamoja na Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT) Said Kiganja.
 Waziri Mwakyembe akigawa vifaa vilivyotolewa na Coca-Cola kwa moja ya mwakilishi wa mmoja wa shule za sekondari.
 Waziri Mwakyembe akikagua moja ya timu wakati wa hafla ya uzinduzi.
 Wadau wa Umisseta katika picha ya pamoja na Waziri Mwakyembe.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...