Na Victor  Masangu, Kisarawe
WAZIRI wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa  (TAMISEMI)  Selemean Jafo amekemea vitendo vinavyofanywa na baadhi ya jamii kuwabagua na kuwanyanyasa  makundi ya watu  wenye ulemavu na  badala yake wabadilike na kuwashirikisha kikamilifu katika shughuli zote  za kimaendeleo sambamba na kuwapatia  fursa za ajira katika sekta mbali mbali  ili waweze kujikwamua kiuchumi pamoja na kuondokana na wimbi la umasikini.

Jafo ametoa kauli hiyo  wakati wa sherehe za ugawaji wa vifaaa saidizi  kwa watu wenye ulemavu wa aina mbali mbali wanaotoka katika halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Mkoa wa Pwani na kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali pamoja na wadau wa wengine wa maendeleo.

 Katika hatua nyingine  Waziri Jafo alimuagiza Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kuhakikisha anawakatia walemavu wote bima ya afya ili waweze kutibiwa bure ili   kuondokana na usumbufu ambao wamekuwa wakiupata, na kuongeza kuwa atatoa kipaumbele cha kwanza kwa watu  wenye umelamvu katika fursa za ajira zilizotangazwa na serikali.
 WAZIRI wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa  (TAMISEMI)  Selemean Jafo (kushoto) akimkabidhi fimbo maalumu kwa ajili ya kutembelea mmoja wa watu wenye ulemavu wa macho, kulia katika halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa halfa ya kukabidhi vifaa saidizi vikiwemo baiskeli za miguu mitatu zipatazo 40, viti  vya mwendo 15 pamoja na fimbo 100.
  WAZIRI wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa  (TAMISEMI)  Selemean Jafo  (aliyevaa suti nyeusi) akimkabidhi fimbo maalumu kwa ajili ya kutembelea mmoja wa watu wenye ulemavu wa macho,kulia katika halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa halfa ya kukabidhi vifaa saidizi vikiwemo baiskeli za miguu mitatu zipatazo 40,viti  vya mwendo 15 pamoja na fimbo 100.
  Mwenyekiti wa Shirikisho la wa wenye ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) Ummy Ndariananga akitoa taarifa kwa mgeni rasmi kuhusina na changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali.
  Mkuu wa Wilaya ya  Kisarawe Happiness Seneda akizngumza na walemavu na baadhi ya wananchi ambao walifika katika hafla ya ugawaji wa vifaa hivyo.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akiuzungumza katika halfa ya ugawaji wa vifaa hivyo kwa watu wenye ulemavu katika  halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe.(Picha Na Victor  Masangu)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...