BODI ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA), ikiongozwa na Mwenyekiti wake Meja Jenerali Mstaafu Hamis Semfuko imefanya ziara ya kujionea shughuli za uhifadhi na juhudi za kudhibiti wa vitendo vya ujangiri zinazodaiwa kufanywa na mwekezaji Mwiba Holding aliyepo Pori la Akiba Maswa lililopo wilayani Meatu mkoani Simiyu. 

Mbali ya kujionea vifaa vya kisasa vya kukabiliana na ujangiri anavyotumia mwekezaji Mwiba Holding, Mwenyekiti wa Bodi akiwa ameongozana na wajumbe wake pia alitembelea kambi ya askari wa doria na kujionea changamoto na mafanikio kadhaa. 

Akizungumza na askari hao amewataka kufanya kazi kwa bidii kwani tayari Bodi yake imefanyia uamuzi baadhi ya masuala ili kuruhusu mabadiliko ya kimfumo wa uendeshaji Mamlaka hiyo. 
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka akizungumza na wanahabari ofisini kwake mjini Bariadi juzi kuhusu umuhimu uhifadhi kupitia Pori ya Akiba Maswa linavyochangia maendeleo hususani sekta ya elimu na afya kwa wananchi
 Mkuu wa Shule ya Sekondari Simiyu Paul Susu akiwaonyesha maofisa wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori nchini (TAWA) na maofisa Elimu Mkoa shughuli za ufyatuaji tofali ambao fedha zake zilichangiwa na TAWA kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na ofisi za shule ya vipaji maalumu ya  Sekondari ya Ufundi Simiyu inayojengwa mjini Bariadi.
 Meneja wa Pori la Akiba Maswa Lusato Masinde akiwaonyesha wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA) pichani mazingira yalipo kambi ya askari wanaoshiriki kufanya doria kwenye pori hilo upande wa Kijiji cha Butuli wilayani Meatu mkoani Simiyu.

 Mkurugenzi wa Utalii Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori nchini (TAWA), Iman Nkui akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa Bodi ya mamlaka hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wake mwenye koti jeusi Meja Jenerali Mstaafu Hamis Semfuko.
 Mjumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori nchini (TAWA), Luteni Jenerali Mstaafu Samweli Ndomba akizungumza na askari waliopo Pori la Akiba Maswa wilayani Meatu mkoani Simiyu kuhusu kujituma na kuibenda kazi yao.
 Mkurugenzi wa Utalii Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori nchini (TAWA), Iman Nkui akitoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo wakati Mwenyekiti wa Bodi ya TAWA Meja Jenerali alipotembelea na kujionea changamoto zinazowakabili akari katika Pori la Akiba Maswa lililopo wilaani Meatu mkoani Smiyu, aliongozana na wajumbe wa bodi hiyo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori nchini (TAWA),  Meja Jenerali Hamis Semfuko akizungumza na akari wa Pori la Akiba Maswa lililopo wilayani Meatu mkoani Simiyu, kushoto kwake ni Mjumbe wa Bodi hiyo Luteni Jenerali Mstaafu Samweli Ndomba na pembeni ni Meneja wa pori hilo Lusato Masinde.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...