Habari
tulizozipata Globu ya Jamii hivi punde kutoka mkoani Kigoma mapema leo
asubuhi hii ya Jumatano Juni 6,2018, inaelezwa kuwa Basi la Hamida
Trans lenye namba za usajili T 885 DLD lililokuwa likitoka Kigoma kwenda
wilaya ya Nzega mkoani Tabora limegonga treni ya mizigo (Garimoshi la
mizigo) katika eneo la Gungu Mjini Kigoma.
Ripota
wetu Editha Karlo aliyekuwepo eneo la tukio na kushuhudia mandhari
halisi ya jali hiyo,ameeleza kuwa ajali hiyo imetokea leo alfajiri, na
mpaka sasa kwa taarifa za awali inaelezwa kuwa Watu 11 wanahofiwa kupoteza maisha,huku idadi ya majeruhi ikidaiwa kuwa ni 26.
Ripota wetu yupo eneo la tukio,hivyo tutaendelea kuwaleta habari kadiri ya zitakavyokuwa zikiingia.
Baadhi ya majeruhi wa ajali wakiendelea na matibabu katika hospitali ya mkoa wa kigoma.
Ripota wetu yupo eneo la tukio,hivyo tutaendelea kuwaleta habari kadiri ya zitakavyokuwa zikiingia.
Baadhi ya Askari wa JWTZ wakiwa tayari wamefika eneo la tukio kwa ajili ya kutoa msaada kwa namna moja ama nyingine
Baadhi
ya Wananchi waliofika kushuhudia tukio la ajali hiyo wakishuhudia
majeruhi wakipakizwa kwenye gari ya Wagonjwa ya JWTZ tayari kupewa
huduma ya kwanza na baadae kupelekwa hospitali kwa matibabu zaidi
Mbunge wa Kigoma mjini Mhe.Zitto Kabwe akiwa eneo la tukio la ajali akishuhudia majeruhi wakiokolewa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...