Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) kimesaini mkataba wa ushirikiano wa miaka mitatu na Asasi ya Habari za Maendeleo Tanzania (TADIO), ambayo pia ni mtandao wa radio zenye maudhui ya kijamii nchini. Mtandao huu una radio 31 wanachama zilizopo Tanzania bara na visiwani.
Chini ya mkataba huo, OUT itatumia wataalam wake (wahadhiri) kushiriki katika vipindi mbalimbali vyenye manufaa kwa umma wa watanzania hususan wananchi wanaoishi vijijni, ambapo radio jamii zinafanya shughuli zake. Pia TADIO kupitia radio wanachama, itawajibika kurusha vipindi hivyo kwa lengo la kuchochea mabadiliko chanya.
Mkataba huo unaipa fursa TADIO kuwa na ofisi zake katika majengo ya Makao Makuu ya Chuo Kikuu Huria, Kinondoni Dar es Salaam. Pia unatoa fursa kwa wanafunzi wa OUT wa taaluma ya habari na mawasiliano, kutumia studio zilizopo katika majengo hayo zinazomilikiwa na TADIO kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo.
Pamoja na kutumia studio hiyo, wanafunzi wa OUT watapata pia nafasi ya kushiriki mafunzo kwa vitendo katika radio wananchama zilizopo katika maeneo mbalimbali nchini.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Prof. Elifas Bisanda akitoa rai juu ya mkataba huo amesema “OUT itatumia mtandao wa radio wanachama wa TADIO kuifikia jamii na kutoa suluhisho la changamoto mbalimbali za kiuchumi na maendeleo zilizopo kwa kuzingatia vigezo vya utafiti.
Mwenyekiti
wa Mtandao wa Asasi ya Habari za Maendeleo (TADIO), Ndg. Prosper
Kwigize (wa pili kulia) akizungumza kabla ya kutiliana saini mkataba wa
ushirikiano wa miaka mitatu na Chuo Kikuu Huria (OUT) wakati wa hafla
fupi iliyofanyika Chuoni hapo jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha
kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha UNESCO
Bi. Nancy Kaizilege, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria (OUT), Profesa
Elifas Bisanda pamoja na Katibu wa Mtandao wa Asasi ya Habari za
Maendeleo (TADIO), Marco Mipawa (kulia).
Mwenyekiti
wa Mtandao wa Asasi ya Habari za Maendeleo (TADIO), Ndg. Prosper
Kwigize na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria (OUT), Profesa Elifas Bisanda
wakibadilishana hati za mkataba wa makubaliano ya ushirikiano kati ya
Chuo Kikuu Huria (OUT) na TADIO wakati wa hafla fupi iliyofanyika chuoni
hapo jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Katibu wa
Mtandao wa Asasi ya Habari za Maendeleo (TADIO), Marco Mipawa (kulia).
Mwenyekiti
wa Mtandao wa Asasi ya Habari za Maendeleo (TADIO), Ndg. Prosper
Kwigize na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria (OUT), Profesa Elifas Bisanda
wakionyesha hati za mkataba wa makubaliano ya ushirikiano kati ya Chuo
Kikuu Huria (OUT) na TADIO mara baada ya kusainiwa wakati wa hafla fupi
iliyofanyika chuoni hapo jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo
ni Katibu wa Mtandao wa Asasi ya Habari za Maendeleo (TADIO), Marco
Mipawa (kulia).
Picha
ya pamoja ya viongozi wa TADIO, UNESCO na OUT baada ya hafla fupi ya
utiaji saini wa mkataba wa makubaliano ya ushirikiano baina ya OUT na
TADIO. Kutoka kushoto walioketi ni Bi. Nancy Kaizilege (UNESCO), Prof
Elifas Bisanda (VC OUT), Prosper Kwigize (Mwenyekiti TADIO) na Marco
Mipawa (Katibu TADIO)
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...