Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii 

Aliyekuwa Mshambuliaji wa timu ya Mbao FC msimu uliopita, Habib Kyombo leo amesaini mkataba wa miaka mitatu na Singida United.

Kyombo ambaye ameitumikia Mbao FC kwa mwaka mmoja na nusu alifanikiwa kufunga mabao 16 kwenye mashindano yote aliyocheza akiwa na timu hiyo. 

Ujumbe wa shukrani aliondika kupitia mtandao, amesema anawashukuru Mbao FC na mashabiki wake, kwa kusema kuwa tangu amevaa Jezi ya timu hiyo  walimpa sapoti yakutosha. 

Bila kusahau amemshukuru, Aliyekuwa Kocha wa timu ya Mbao, Ettiene Ndayirajige kwa imani yake nakuonyesha kumuamini katika nafasi ya ushambuliaji ambao imesaidia kumsogeza karibu na ndoto zake. 

Amesema hatosahau na itabaki kumbukumbu kwake baada yakuisaidia timu hiyo kufika Fanali ya Michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) msimu uliopita ambapo walipoteza kwa kichapo cha bao 2-1 mbele ya Simba SC.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...