UTANGULIZI

Shukrani
  1. Mheshimiwa Spika, awali ya yote namshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutufikisha siku hii ya leo tukiwa na afya njema ambapo tunahitimisha Mkutano wa 11 ulioanza Jumanne tarehe 3 Aprili 2018.

  1. Mheshimiwa Spika, nakushukuru wewe binafsi, Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wenyeviti wa Bunge na Waheshimiwa Wabunge wote kwa kushiriki kikamilifu katika mkutano huu tangu tulipoanza vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge na baadaye Mkutano wa Bunge. Katika mkutano huu, tumeweza kutekeleza kikamilifu wajibu wetu wa Kikatiba kwa kujadili na kupitisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2018/2019. Mtakubaliana nami kuwa Bajeti hii inatoa mwelekeo mzuri wa utekelezaji wa ahadi mbalimbali za Serikali kwa wananchi, kama zilivyoainishwa kupitia Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015 – 2020 pamoja na maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akifungua rasmi Bunge la Kumi na Moja tarehe 20 Novemba 2015.

Salamu za Pole
Mheshimiwa Spika, tarehe 26 Mei, 2018 Bunge lako tukufu lilipokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mheshimiwa Kasuku Samson Bilago, aliyekuwa Mbunge wa Buyungu, Kigoma. Nitumie nafasi hii kukupa pole wewe binafsi Mheshimiwa Spika, Bunge lako tukufu, Mke, Watoto, familia ya marehemu na wananchi wote wa Buyungu kwa kumpoteza mwakilishi wao huyo aliyekuwa na mchango mzuri kwenye Bunge letu tukufu. Vilevile, nitumie fursa hii kutoa salamu za pole kwa Mheshimiwa Stephen Hillary Ngonyani Mbunge wa Korogwe Vijijini na Mheshimiwa Angelina Sylvester Mabula, Mbunge wa Ilemela, Mwanza, kwa kufiwa na wenza wao.
Kusoma hotuba yote BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...