Mkuu wa Jeshi la Polisi
Nchini IGP Simon Sirro akiwa na baadhi ya wananchi na abiria waliokuwa
safarini wakisaidiana kuokoa majeruhi kutoka kwenye roli aina ya Scania lenye
namba T 396 CCY iliyokuwa ikitokea Morogoro kuelekea Dar es salaam baada ya kupata
ajali na kuanguka katika eneo la Bwawani mkoani Morogoro na kusababisha
majeruhi mmoja ambaye ni dereva wa roli hilo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi
Nchini IGP Simon Sirro (wa Pili kulia), akiwa na dereva wa roli aina ya Scania (wa pili kushoto) aliyeokolewa muda
mfupi uliopita kutoka kwenye roli alilokuwa akiliendesha baada ya kupata ajali na
kuanguka katika eneo la Bwawani mkoani Morogoro na kusababisha majeruhi mmoja
ambaye ni dereva wa roli hilo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi
Nchini IGP Simon Sirro, akisalimiana na kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma SACP
Gilles Muroto, muda mfupi baada ya kuwasili mkoani humo kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi
Nchini IGP Simon Sirro (katikati), akizungumza na kamanda wa Polisi mkoa wa
Dodoma SACP Gilles Muroto na kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Kamishna
Msaidizi wa Polisi (ACP) Mugabo Wekwe alipokutananao katika mpaka
unaotenganisha mkoa wa Morogoro na Dodoma kabla ya kuwasili mkoani Dodoma kwa
ziara ya kikazi. Picha na Jeshi la
Polisi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...